Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tunapaswa Kuwatendea Wengine Jinsi Gani?
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Mei 15
    • 12. (a) Yesu alisema nini kuhusu nuru ya kiroho? (b) Tunaweza kuacha nuru yetu iangaze jinsi gani?

      12 Tunawatendea watu kwa njia bora zaidi tunapowasaidia kupata nuru ya kiroho kutoka kwa Mungu. (Zab. 43:3) Yesu aliwaambia wanafunzi wake kwamba walikuwa “nuru ya ulimwengu” naye aliwahimiza waache nuru yao iangaze ili watu waweze kuona ‘matendo yao mazuri’ kuelekea wengine. Kwa kufanya hivyo, wangeangaza nuru ya kiroho “mbele ya watu,” au kwa faida ya wanadamu. (Soma Mathayo 5:14-16.) Leo, tunaacha nuru yetu iangaze kwa kuwatendea mema majirani wetu na kushiriki katika kazi ya kuhubiri habari njema “katika ulimwengu wote,” yaani, “katika mataifa yote.” (Mt. 26:13; Marko 13:10) Tuna pendeleo kubwa kama nini!

  • Tunapaswa Kuwatendea Wengine Jinsi Gani?
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Mei 15
    • 15. ‘Matendo yetu mazuri’ yanakuwa na uvutano gani juu ya watu fulani?

      15 Baada ya kusema kuhusu taa inayowaka, Yesu aliwaambia hivi wanafunzi wake: “Vivyo hivyo acheni nuru yenu iangaze mbele ya watu, ili wapate kuona matendo yenu mazuri na kumpa utukufu Baba yenu aliye mbinguni.” Kwa sababu ya ‘matendo yetu mazuri,’ watu fulani ‘wanampa Mungu utukufu’ kwa kuwa watumishi wake. Tunachochewa kama nini kuendelea ‘kuangaza kama mianga katika ulimwengu’!—Flp. 2:15.

      16. Kwa kuwa sisi ni “nuru ya ulimwengu,” tunapaswa kufanya nini?

      16 Kwa kuwa sisi ni “nuru ya ulimwengu,” tunapaswa kushiriki katika kazi ya kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi. Lakini tunahitaji kufanya jambo lingine. Mtume Paulo aliandika hivi: “Endeleeni kutembea kama watoto wa nuru, kwa maana matunda ya nuru yana kila namna ya wema na uadilifu na kweli.” (Efe. 5:8, 9) Sikuzote tunapaswa kuweka mfano mzuri kupitia mwenendo wetu unaompendeza Mungu. Kwa kweli, tunapaswa kutii shauri hili la mtume Petro: “Dumisheni mwenendo wenu ukiwa mzuri katikati ya mataifa, ili, katika jambo ambalo wanasema juu yenu ya kuwa ninyi ni watenda-maovu, waweze, likiwa tokeo la matendo yenu mazuri ambayo wameshuhudia kwa macho, kumtukuza Mungu katika siku ya ukaguzi wake.” (1 Pet. 2:12) Lakini ni hatua gani tunayopaswa kuchukua ikiwa uhusiano wetu na mwamini mwenzetu si mzuri?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki