-
Uadilifu Si kwa Mapokeo ya MdomoMnara wa Mlinzi—1990 | Oktoba 1
-
-
‘Mlisikia Kwamba Ilinenwa’
-
-
Uadilifu Si kwa Mapokeo ya MdomoMnara wa Mlinzi—1990 | Oktoba 1
-
-
13. Yesu aonyaje hata dhidi ya mwanzo wa mwenendo ambao ungeweza kuongoza kwenye uuaji halisi?
13 Sasa fikiria ya kwanza ya mfululizo huu wa taarifa sita. Yesu alijulisha rasmi hivi: “Mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiue; na mtu akiua, itampasa hukumu. Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye [aendeleaye kumwonea, NW] ndugu yake hasira itampasa hukumu.” (Mathayo 5:21, 22) Kasirani katika moyo yaweza kuongoza kwenye matusi na kutoka hapo iongoze kwenye hukumu za laana, na hatimaye huenda ikaongoza kwenye kitendo chenyewe cha kuua. Kasirani yenye kukuzwa kwa muda mrefu moyoni yaweza kuwa hatari: “Kila amchukiaye ndugu yake ni mwuaji.”—1 Yohana 3:15.
-