-
Tunawezaje Kuwa Safi Machoni pa Mungu?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
4. Shinda mazoea mabaya
Yehova anaweza kutusaidia kushinda zoea lolote baya
Ikiwa wewe ni mraibu wa kuvuta sigara au kutumia dawa za kulevya, huenda unaelewa jinsi ilivyo vigumu kushinda mazoea hayo. Ni nini ambacho kitakusaidia? Fikiria madhara unayopata kutokana na mazoea hayo. Soma Mathayo 22:37-39, kisha mzungumzie jinsi kuvuta sigara au kutumia dawa za kulevya kunavyoathiri . . .
urafiki wa mtu na Yehova.
familia ya mtu huyo na watu wanaomzunguka.
Chukua hatua ambazo zitakusaidia kushinda mazoea mabaya.a Onyesha VIDEO.
Soma Wafilipi 4:13, kisha mzungumzie swali hili:
Kuwa na mazoea mazuri ya kusali, kujifunza Biblia, na kuhudhuria mikutano kunawezaje kumsaidia mtu apate nguvu za kushinda mazoea mabaya?
5. Jitahidi kushinda mawazo na mazoea machafu
Soma Wakolosai 3:5, kisha mzungumzie maswali haya:
Tunajuaje kwamba kutazama ponografia, kutuma ujumbe au picha za ngono, na kupiga punyeto ni mazoea machafu machoni pa Yehova?
Je, inawezekana kufuata sheria za Yehova kuhusu usafi wa maadili? Kwa nini?
Jifunze jinsi ya kushinda mawazo machafu. Onyesha VIDEO.
Yesu alitoa mfano unaoonyesha kwamba tunapaswa kuchukua hatua thabiti ili tuendelee kudumisha maadili safi. Soma Mathayo 5:29, 30, kisha mzungumzie swali hili:
Ingawa Yesu hakumaanisha tunapaswa kujisababishia majeraha ya kimwili, alionyesha kwamba tunapaswa kuchukua hatua fulani. Mtu anapaswa kuchukua hatua gani thabiti ili kuepuka mawazo machafu?b
Ikiwa unapambana ili kushinda mawazo machafu, Yehova anathamini jitihada zako. Soma Zaburi 103:13, 14, kisha mzungumzie swali hili:
Ikiwa unapambana na zoea chafu, andiko hili linawezaje kukusaidia uendelee kupambana?
Usife moyo, endelea kupambana!
Huenda ukajiambia hivi, ‘Nimeshindwa, hakuna haja ya kuendelea kupambana.’ Lakini fikiria jambo hili: Mkimbiaji anapoanguka haimaanishi kwamba hawezi kuendelea na mbio hizo, pia haimaanishi kwamba anapaswa kurudi nyuma na kuanza tena. Vivyo hivyo, hata unapolemewa na kurudia zoea hilo, haimaanishi kwamba huwezi kulishinda. Wala haimaanishi kwamba jitihada ulizofanya ni za bure. Ni jambo la kawaida kujikwaa. Lakini usife moyo! Kwa msaada wa Yehova, unaweza kushinda zoea baya.
-
-
Wakristo Wanapaswa Kuwa na Maoni Gani Kuhusu Kileo?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
6. Jinsi ya kushinda zoea la kunywa kupita kiasi
Ona jambo lililomsaidia mwanamume fulani ashinde zoea la kunywa kileo kupita kiasi. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.
Katika video hiyo, Dmitry alitendaje baada ya kunywa kileo?
Je, ilikuwa rahisi kwake kuacha mara moja zoea hilo?
Mwishowe, nini kilichomsaidia kushinda uraibu wa kunywa kileo?
Soma 1 Wakorintho 6:10, 11, kisha mzungumzie maswali haya:
Kwa nini ulevi ni kosa zito?
Ni nini kinachoonyesha kwamba mtu aliye na zoea la kunywa kupita kiasi anaweza kubadilika?
Soma Mathayo 5:30, kisha mzungumzie swali hili:
Kukata mkono kunamaanisha kwamba mtu anapaswa kuacha tabia fulani ili amfurahishe Yehova. Unaweza kufanya nini ikiwa unapambana kushinda zoea la kunywa kileo kupita kiasi?a
Soma 1 Wakorintho 15:33, kisha mzungumzie swali hili:
Rafiki zako wanawezaje kufanya unywe kileo kupita kiasi?
-