-
Uadilifu Si kwa Mapokeo ya MdomoMnara wa Mlinzi—1990 | Oktoba 1
-
-
‘Mlisikia Kwamba Ilinenwa’
-
-
Uadilifu Si kwa Mapokeo ya MdomoMnara wa Mlinzi—1990 | Oktoba 1
-
-
15. Msimamo wa Yesu juu ya talaka ulitofautianaje kabisa na ule uliosimuliwa katika mapokeo ya mdomo ya Wayahudi?
15 Sasa twaja kwenye taarifa ya tatu ya Yesu. Alisema hivi: “Imenenwa pia, Mtu akimwacha mkewe, na ampe hati ya talaka; lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye [akimtaliki, NW] mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa [aliyetalikiwa, NW, yaani, aliyetalikiwa kwa sababu zisizo ukosefu wa adili katika ngono], azini.” (Mathayo 5:31, 32) Wayahudi fulani wali-shughulika na wake zao kwa hila na wakawataliki kwa visababu hafifu kabisa. (Malaki 2:13-16; Mathayo 19:3-9) Mapokeo ya mdomo yaliruhusu mwanamume kutaliki mke wake “hata ikiwa alimharibia mapishi” au “ikiwa alipata mwingine mrembo kuliko yeye.”—Mishnah.
-