-
Uadilifu Si kwa Mapokeo ya MdomoMnara wa Mlinzi—1990 | Oktoba 1
-
-
15. Msimamo wa Yesu juu ya talaka ulitofautianaje kabisa na ule uliosimuliwa katika mapokeo ya mdomo ya Wayahudi?
15 Sasa twaja kwenye taarifa ya tatu ya Yesu. Alisema hivi: “Imenenwa pia, Mtu akimwacha mkewe, na ampe hati ya talaka; lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye [akimtaliki, NW] mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa [aliyetalikiwa, NW, yaani, aliyetalikiwa kwa sababu zisizo ukosefu wa adili katika ngono], azini.” (Mathayo 5:31, 32) Wayahudi fulani wali-shughulika na wake zao kwa hila na wakawataliki kwa visababu hafifu kabisa. (Malaki 2:13-16; Mathayo 19:3-9) Mapokeo ya mdomo yaliruhusu mwanamume kutaliki mke wake “hata ikiwa alimharibia mapishi” au “ikiwa alipata mwingine mrembo kuliko yeye.”—Mishnah.
-
-
Uadilifu Si kwa Mapokeo ya MdomoMnara wa Mlinzi—1990 | Oktoba 1
-
-
19. Yesu alipendekeza tufuate tendo gani la Yehova kuelekea waovu?
19 Akiendelea na mahubiri yake, Yesu alipiga mbiu kwamba ‘Mungu alionyesha upendo kwa waovu. Alisababisha jua liwaangazie na mvua iwanyeshee. Hakuna jambo lolote la ajabu katika kupenda wale wakupendao. Waovu hufanya hivyo. Hakuna sababu ya kuthawabishwa kwa jambo hilo. Jithibitisheni kuwa wana wa Mungu. Mwigeni. Jifanye uwe jirani wa wote na umpende jirani yako. Na hivyo mwe “wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.”’ (Mathayo 5:45-48) Lo, ni wito wa ushindani kama nini kuishi kwa kutimiza kiwango hicho! Nacho chaonyesha upungufu mkubwa kama nini wa uadilifu wa waandishi na Mafarisayo!
-