-
Uadilifu Si kwa Mapokeo ya MdomoMnara wa Mlinzi—1990 | Oktoba 1
-
-
16. Ni zoea gani la Kiyahudi lililofanya kuapa viapo kukose maana, na Yesu alichukua msimamo gani?
16 Kwa kufuata ukanda ule ule Yesu aliendelea hivi: “Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usizuri [usiape bila kufanya, NW] . . . lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa.” Kufikia wakati huu Wayahudi walikuwa wakivunja heshima ya kiapo wakawa wakiapa-apa viapo vingi juu ya vijambo visivyo vya maana bila kuvifanya. Lakini Yesu alisema: “Usiape kabisa . . . Bali maneno yenu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo.” Kanuni yake ilikuwa sahili: Sema ukweli nyakati zote, bila kulazimika kuhakikisha neno lako kwa kiapo. Acha viapo vibakie kwa mambo yaliyo muhimu.—Mathayo 5:33-37; linganisha 23:16-22.
-
-
Uadilifu Si kwa Mapokeo ya MdomoMnara wa Mlinzi—1990 | Oktoba 1
-
-
19. Yesu alipendekeza tufuate tendo gani la Yehova kuelekea waovu?
19 Akiendelea na mahubiri yake, Yesu alipiga mbiu kwamba ‘Mungu alionyesha upendo kwa waovu. Alisababisha jua liwaangazie na mvua iwanyeshee. Hakuna jambo lolote la ajabu katika kupenda wale wakupendao. Waovu hufanya hivyo. Hakuna sababu ya kuthawabishwa kwa jambo hilo. Jithibitisheni kuwa wana wa Mungu. Mwigeni. Jifanye uwe jirani wa wote na umpende jirani yako. Na hivyo mwe “wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.”’ (Mathayo 5:45-48) Lo, ni wito wa ushindani kama nini kuishi kwa kutimiza kiwango hicho! Nacho chaonyesha upungufu mkubwa kama nini wa uadilifu wa waandishi na Mafarisayo!
-