-
Uadilifu Si kwa Mapokeo ya MdomoMnara wa Mlinzi—1990 | Oktoba 1
-
-
17. Yesu alifundisha kufuata njia gani bora kuliko “jicho kwa jicho, na jino kwa jino”?
17 Ndipo Yesu akasema: “Mmesikia kwamba imenenwa, Jicho kwa jicho, na jino kwa jino; lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili.” (Mathayo 5:38-42) Hapa Yesu harejezei pigo lenye madhumuni ya kuumiza bali kofi la madharau kwa kutumia upande wa nyuma wa mkono. Wewe mwenyewe usijishushie hadhi kwa kurudisha madharau. Kataa kurudisha ovu kwa ovu. Bali, rudisha wema na hivyo “uushinde ubaya kwa wema.”—Warumi 12:17-21.
-
-
Uadilifu Si kwa Mapokeo ya MdomoMnara wa Mlinzi—1990 | Oktoba 1
-
-
19. Yesu alipendekeza tufuate tendo gani la Yehova kuelekea waovu?
19 Akiendelea na mahubiri yake, Yesu alipiga mbiu kwamba ‘Mungu alionyesha upendo kwa waovu. Alisababisha jua liwaangazie na mvua iwanyeshee. Hakuna jambo lolote la ajabu katika kupenda wale wakupendao. Waovu hufanya hivyo. Hakuna sababu ya kuthawabishwa kwa jambo hilo. Jithibitisheni kuwa wana wa Mungu. Mwigeni. Jifanye uwe jirani wa wote na umpende jirani yako. Na hivyo mwe “wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.”’ (Mathayo 5:45-48) Lo, ni wito wa ushindani kama nini kuishi kwa kutimiza kiwango hicho! Nacho chaonyesha upungufu mkubwa kama nini wa uadilifu wa waandishi na Mafarisayo!
-