-
Wanajimu Wamtembelea YesuYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Watu fulani wanakuja kutoka Mashariki. Ni wanajimu—watu wanaochunguza nyota, wakidai kwamba wakifanya hivyo wanaweza kujua maana ya matukio yanayohusu maisha ya watu. (Isaya 47:13) Wakiwa nyumbani kwao huko Mashariki, waliona “nyota” na kuifuata mamia ya kilomita hadi Yerusalemu, badala ya kwenda Bethlehemu.
Wanajimu hao wanapofika huko, wanauliza: “Yuko wapi yule aliyezaliwa awe mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake tulipokuwa Mashariki, nasi tumekuja kumsujudia.”—Mathayo 2:1, 2.
-
-
Wanajimu Wamtembelea YesuYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Unafikiri ni nani aliyefanya “nyota” hiyo iwaongoze wanajimu? Kumbuka, haikuwaongoza moja kwa moja hadi kwa Yesu huko Bethlehemu. Badala yake iliwaongoza hadi Yerusalemu, ambako walikutana na Mfalme Herode aliyetaka kumuua Yesu. Na angefanya hivyo ikiwa Mungu hangeingilia kati kuwaonya wanajimu hao wasimwonyeshe Herode mahali ambapo Yesu alikuwa. Ni wazi kwamba adui wa Mungu, Shetani, ndiye aliyetaka Yesu auawe, na alitumia njia hiyo kujaribu kutimiza kusudi lake.
-