Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tunapaswa Kusali kwa Mungu Jinsi Gani?
    Amkeni!—2012 | Februari
    • Yesu alisema: “Basi, ninyi msali hivi: ‘Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe. Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni. Utupe leo mkate wetu kwa ajili ya siku hii; na utusamehe madeni yetu, kama vile ambavyo sisi pia tumewasamehe wadeni wetu. Na usituingize katika jaribu, bali utukomboe kutokana na yule mwovu.’”​—Mathayo 6:9-13.

  • Tunapaswa Kusali kwa Mungu Jinsi Gani?
    Amkeni!—2012 | Februari
    • “Ufalme wako na uje.” Ufalme wa Mungu ni serikali iliyo chini ya Yesu Kristo, ambaye ndiye Mfalme wake. Hivi karibuni ataitawala dunia yote. Danieli 7:14 inasema hivi: “Naye akapewa utawala na heshima na ufalme.” Ufalme wa Mungu ‘utakuja’ wakati utakapoingilia shughuli za wanadamu na kuziponda tawala zote zinazoupinga na kuchukua mamlaka duniani pote.​—Danieli 2:44.

      “Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.” Chini ya utawala wa Ufalme, wanadamu watajitiisha kwa mapenzi ya Mungu. Kwa sababu hiyo, kutakuwa na amani ya kweli na wanadamu wote watamwabudu Mungu kupatana na mapenzi yake. Siasa na dini ya uwongo ambayo huleta migawanyiko haitakuwepo tena. Kwa njia ya mfano, “hema la Mungu” litakuwa “pamoja na wanadamu,” inasema Ufunuo 21:3, 4, “naye atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki