Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sala Ambazo Hakika Zitajibiwa
    Mnara wa Mlinzi—1991 | Septemba 15
    • KUNA sala ambazo zitajibiwa pasipo shaka. Wazo kuu la sala hizo limo katika kiolezo ambacho Yesu Kristo aliwapa wanafunzi wake aliposema: “Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe [litakaswe, NW], ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.”—Mathayo 6:9-13.

  • Sala Ambazo Hakika Zitajibiwa
    Mnara wa Mlinzi—1991 | Septemba 15
    • “Ufalme Wako Uje”

      Yesu aliwaambia wafuasi wake wasali hivi pia: “Ufalme wako uje.” Pasipo shaka sala za kuomba kuja kwa Ufalme wa Mungu zitajibiwa. Ufalme ni utawala wa enzi kuu ya Yehova kama uonyeshwavyo kupitia serikali ya kimbingu ya Kimesiya ikiwa mikononi mwa Mwana wake, Yesu Kristo, na “watakatifu” walio washirika. (Danieli 7:13, 14, 18, 22, 27; Isaya 9:6, 7) Kwa muda mrefu Mashahidi wa Yehova wamethibitisha kutokana na Maandiko kwamba Yesu alitawazwa akiwa Mfalme wa kimbingu katika mwaka 1914. Basi, kwa nini impase mtu yeyote kusali ili Ufalme “uje”?

      Kusali ili kuomba kuja kwa Ufalme kwa kweli humaanisha kuomba kwamba uje dhidi ya wapinzani wote wa utawala wa kimungu duniani. Karibuni sasa “ufalme [wa Mungu] . . . utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.” (Danieli 2:44) Tukio hilo litachangia utakaso wa jina takatifu la Yehova.

      “Mapenzi Yako Yatimizwe”

      Yesu alizidi kufundisha wanafunzi wake kusali hivi: “Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.” Hilo ni ombi la kwamba Yehova atende kupatana na mapenzi yake kwa dunia. Lafanana na julisho la mtunga zaburi: “BWANA [Yehova, NW] amefanya kila lililompendeza, katika mbingu na katika nchi, katika bahari na katika vilindi vyote. Ndiye apandishaye mvuke toka miisho ya nchi; huifanyia mvua umeme; hutoa upepo katika hazina zake. Aliwapiga wazaliwa wa kwanza wa Misri, wa wanadamu na wa wanyama. Alipeleka ishara na maajabu kati yako, Ee Misri, juu ya Farao na watumishi wake wote. Aliwapiga mataifa mengi, akawaua wafalme wenye nguvu.”—Zaburi 135:6-10.

      Kusali kwamba mapenzi ya Yehova yatimizwe duniani ni ombi la kwamba atekeleze makusudi yake kuelekea tufe hili. Hiyo yatia ndani kuondoshwa daima kwa wapinzani wake, kama vile alivyowaondoa kwa kadiri ndogo nyakati za kale. (Zaburi 83:9-18; Ufunuo 19:19-21) Sala za kuomba mapenzi ya Yehova yafanywe katika sehemu zote za dunia na katika ulimwengu wote mzima hakika zitajibiwa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki