Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi Unavyoweza Kupata Mafanikio ya Kweli Maishani
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Desemba 15
    • 13. Yesu alitoa shauri gani kuhusu kujiwekea hazina?

      13 Yesu alisema hivi kuhusu hazina: “Acheni kujiwekea hazina duniani, ambako nondo na kutu hula, na ambako wezi huvunja na kuiba. Badala yake, jiwekeeni hazina mbinguni, ambako nondo na kutu havili, na ambako wezi hawavunji na kuiba. Kwa maana mahali ilipo hazina yako, ndipo moyo wako utakapokuwa pia.”—Mt. 6:19-21.

  • Jinsi Unavyoweza Kupata Mafanikio ya Kweli Maishani
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Desemba 15
    • 15. Tunapaswa kujitahidi kutafuta mafanikio ya aina gani?

      15 Viongozi fulani wa kidini wamehubiri kwamba ni makosa kujitahidi kufanikiwa na kwamba jitihada zote za kutafuta mafanikio zinapaswa kukomeshwa. Hata hivyo, kumbuka kwamba Yesu hakuwa akishutumu jitihada zote za aina hiyo. Badala yake, alikuwa akiwashauri wanafunzi wake wajitahidi kutafuta mafanikio yanayofaa, akiwahimiza kuweka “hazina [zisizoharibika] mbinguni.” Tamaa yetu kuu inapaswa kuwa kujitahidi kufanikiwa kulingana na maoni ya Yehova. Naam, maneno ya Yesu yanatukumbusha kwamba tuna hiari ya kuchagua mambo tutakayofuatilia. Hata hivyo, ukweli ni kwamba tutafuatilia mambo yaliyo moyoni mwetu, yale tunayothamini.

      16. Tunaweza kuwa na uhakika kabisa katika jambo gani?

      16 Ikiwa kwa kweli tumeazimia moyoni mwetu kumpendeza Yehova, tunaweza kuwa na hakika kwamba atahakikisha tunapata vitu tunavyohitaji. Huenda akaruhusu tupate njaa au kiu kwa muda, kama ilivyokuwa kwa mtume Paulo. (1 Kor. 4:11) Hata hivyo, tunaweza kuwa na uhakika kabisa katika shauri hili la Yesu lenye hekima: “Msihangaike kamwe na kusema, ‘Tutakula nini?’ au, ‘Tutakunywa nini?’ au, ‘Tutavaa nini?’ Kwa maana vyote hivi ndivyo vitu ambavyo mataifa yanafuatilia kwa tamaa. Kwa maana Baba yenu wa mbinguni anajua mnahitaji vitu hivi vyote. Basi, endeleeni kuutafuta kwanza ufalme na uadilifu wake, nanyi mtaongezewa hivi vitu vingine vyote.”—Mt. 6:31-33.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki