Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yesu Afunua “Hekima Kutoka kwa Mungu”
    Mkaribie Yehova
    • 6-8. (a) Yesu anataja sababu zipi nzuri za kuepuka mahangaiko? (b) Ni nini kinachoonyesha kwamba Shauri la Yesu lina hekima ya kutoka juu?

      6 Kwa mfano, fikiria shauri la Yesu lenye hekima katika Mathayo sura ya 6 linaloonyesha jinsi ya kupambana na mahangaiko ya vitu vya kimwili. Yesu anatushauri hivi: “Komeni kuhangaikia nafsi zenu kuhusu ni nini mtakula au ni nini mtakunywa, au juu ya miili yenu kuhusu ni nini mtavaa.” (Mstari wa 25) Chakula na mavazi ni mahitaji ya lazima, na ni jambo la kawaida tu kuhangaikia vitu hivyo. Lakini Yesu anatuambia ‘tukome kuhangaikia’ vitu hivyo.b Kwa nini?

      7 Msikilize Yesu anaposababu kwa njia yenye kusadikisha. Kwa kuwa Yehova ametupatia uhai na mwili, je, anaweza kushindwa kutuandalia chakula cha kuendeleza uhai huo na mavazi ya kujivika? (Mstari wa 25) Ikiwa Mungu anawalisha ndege na kuyapamba maua, basi, hatawatunza zaidi wanadamu wanaomwabudu! (Mstari wa 26, 28-30) Kwa kweli, haifai kuwa na mahangaiko yasiyofaa. Hatuwezi kuongeza muda wetu wa uhai hata kwa dhiraa moja kwa kuhangaika.c (Mstari wa 27) Tunawezaje kuepuka mahangaiko? Yesu anatushauri hivi: Endeleeni kuitanguliza ibada ya Mungu maishani mwenu. Wale wanaofanya hivyo wanaweza kuwa na uhakika kwamba Baba yao wa mbinguni ‘atawaongezea’ mahitaji yao ya kila siku. (Mstari wa 33) Mwishowe, Yesu atoa dokezo nzuri sana—usihangaikie mambo ya kesho. Mbona uzidishe mahangaiko ya leo kwa kuhangaikia mambo ya kesho? (Mstari wa 34) Licha ya hayo, mbona uhangaikie mambo ambayo huenda yasitukie kamwe? Tunaweza kuepuka maumivu makali ya moyoni tukifuata shauri hilo la hekima katika ulimwengu huu uliojaa mikazo.

  • Yesu Afunua “Hekima Kutoka kwa Mungu”
    Mkaribie Yehova
    • b Kitenzi cha Kigiriki kinachotafsiriwa “hangaikia” kinamaanisha “kukengeushwa fikira.” Katika Mathayo 6:25, neno hilo linamaanisha woga na wasiwasi ambao unakengeusha au kupotosha fikira, na kumfanya mtu akose shangwe maishani.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki