-
Yohana Mbatizaji Atayarisha NjiaYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Yohana ni mtu anayevutia sana, kwa jinsi anavyoonekana na kuongea. Nguo zake zimeshonwa kwa manyoya ya ngamia, naye anavaa mshipi wa ngozi kiunoni mwake. Anakula nzige—aina fulani ya panzi—na asali ya porini. Anatangaza ujumbe gani? “Tubuni, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia.”—Mathayo 3:2.
Ujumbe wa Yohana unawasisimua watu wanaokuja kumsikiliza. Wengi wanatambua kwamba wanahitaji kutubu, yaani kubadili mtazamo na mwenendo wao, wakiacha maisha yao ya zamani ambayo hayafai. Wale ambao wamemjia wanatoka “Yerusalemu na Yudea yote na maeneo yote yaliyo karibu na Yordani.” (Mathayo 3:5) Wengi kati ya wale ambao wamekuja kwa Yohana, wanatubu. Anawabatiza kwa kuwazamisha katika maji ya mto Yordani. Kwa nini?
-
-
Yohana Mbatizaji Atayarisha NjiaYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Kwa hiyo, ujumbe wa Yohana, “Tubuni, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia,” ni muhimu sana. (Mathayo 3:2) Ni tangazo la hadharani kwamba huduma ya Yesu Kristo, Mfalme anayekuja ambaye amechaguliwa na Yehova, iko karibu kuanza.
-