-
Mashahidi Wakristo Walio na Uraia wa KimbinguMnara wa Mlinzi—1995 | Julai 1
-
-
2. Yohana Mbatizaji alitangaza jambo jipi jipya ambalo Yesu angefanya, na jambo hili jipya lilihusu nini?
2 Yohana Mbatizaji alipokuwa akimtayarishia Yesu njia, alitangaza kwamba Yesu angefanya jambo fulani jipya. Rekodi yasema: ‘Yohana akahubiri akisema, Yuaja nyuma yangu aliye na nguvu kuliko mimi, ambaye mimi sistahili kuinama na kuilegeza gidamu ya viatu vyake. Mimi niliwabatiza kwa maji; bali yeye atawabatiza kwa roho takatifu.’ (Marko 1:7, 8) Kabla ya wakati huo, hakuna mtu aliyekuwa amebatizwa kwa roho takatifu. Huu ulikuwa mpango mpya unaohusu roho takatifu, nao ulihusisha kusudi la Yehova lililokuwa karibu kufunuliwa la kutayarisha wanadamu kwa ajili ya utawala wa kimbingu.
-
-
Mashahidi Wakristo Walio na Uraia wa KimbinguMnara wa Mlinzi—1995 | Julai 1
-
-
5. Ni wakati gani wafuasi waaminifu walipobatizwa kwa roho takatifu, na ni utendaji gani mbalimbali unaohusika wa roho takatifu uliotokea wakati uo huo?
5 Yesu aliposema na Nikodemo, roho takatifu ilikuwa tayari imekuja juu ya Yesu, ikimtia mafuta kwa ajili ya utawala wake katika Ufalme wa Mungu, na Mungu alikuwa amekiri peupe kwamba Yesu alikuwa Mwana Wake. (Mathayo 3:16, 17) Yehova alizaa watoto wengine zaidi wa kiroho katika Pentekoste 33 W.K. Wanafunzi waaminifu waliokusanyika katika chumba cha juu Yerusalemu walibatizwa kwa roho takatifu. Wakati uo huo, walizaliwa mara ya pili kutokana na roho takatifu kuwa wana wa kiroho wa Mungu. (Matendo 2:2-4, 38; Warumi 8:15) Na zaidi, walitiwa mafuta kwa roho takatifu kwa kusudi la urithi wa kimbingu wa wakati ujao, nao mwanzoni walitiwa muhuri kwa roho takatifu ukiwa wonyesho wa uhakika wa tumaini la kimbingu.—2 Wakorintho 1:21, 22.
-