-
Maisha ya Utotoni Huko NazaretiYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Yesu ameletwa hapa na Yosefu na Maria kutoka Misri labda akiwa na umri wa miaka miwili. Inaonekana wakati huu, yeye ndiye mtoto wao pekee. Hata hivyo, ndugu zake wa kambo wanazaliwa baadaye—Yakobo, Yosefu, Simoni, na Yuda. Pia Yosefu na Maria wanazaa watoto wa kike, dada za kambo wa Yesu. Naam, Yesu ana angalau ndugu na dada sita wadogo.
-
-
Maisha ya Utotoni Huko NazaretiYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Yosefu anahitaji kufanya kazi kwa bidii ili kuitegemeza familia yake inayoongezeka. Yeye ni seremala. Yosefu anamlea Yesu kama mwana wake mwenyewe, hivyo Yesu anaitwa “mwana wa yule seremala.” (Mathayo 13:55) Yosefu pia anamfundisha Yesu kazi ya useremala, naye Yesu anajifunza vizuri sana. Ndiyo maana baadaye watu wanasema hivi kumhusu Yesu: “Je, huyu si yule seremala?”—Marko 6:3.
-