-
Yesu Amponya Mvulana Mwenye Roho MwovuYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Yesu, Petro, Yakobo na Yohana wanaposhuka kutoka mlimani, wanakutana na umati mkubwa. Kuna tatizo. Waandishi wamewazunguka wanafunzi wakibishana nao. Watu wanashangaa kumwona Yesu, nao wanakimbia kwenda kumsalimu. Yesu anawauliza: “Mnabishania nini?”—Marko 9:16.
-
-
Yesu Amponya Mvulana Mwenye Roho MwovuYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Inaonekana waandishi wanawashutumu wanafunzi kwa sababu wameshindwa kumponya mvulana huyo, labda hata wanawadhihaki. Basi badala ya kumjibu baba huyo aliye na wasiwasi, Yesu anauambia umati: “Enyi kizazi kisicho na imani na kilichopotoka, nitaendelea kuwa pamoja nanyi mpaka lini? Nitawavumilia mpaka lini?” Maneno hayo mazito yanawahusu waandishi ambao walikuwa wakiwasumbua wanafunzi wake kabla hajafika. Akimgeukia yule baba aliyehuzunika, Yesu anasema: “Mleteni hapa.”—Mathayo 17:17.
-