-
“Mwacheni Msomaji Atumie Ufahamu”Mnara wa Mlinzi—1999 | Mei 1
-
-
18, 19. Ni sababu zipi zimetolewa kuonyesha kwamba “kukimbilia milimani” hakutamaanisha kubadili dini?
18 Baada ya kutabiri kuhusu ‘kitu chenye kuchukiza sana kikisimama katika mahali patakatifu,’ Yesu aliwaonya wenye ufahamu wachukue hatua. Je, alimaanisha kwamba kufikia wakati huo wa mwisho—wakati ambapo “kitu chenye kuchukiza sana” “kikiwa kimesimama katika mahali patakatifu”—watu wengi wataikimbia dini isiyo ya kweli na kujiunga na ibada ya kweli? Sivyo. Ufikirie utimizo wa kwanza. Yesu alisema hivi: “Waacheni wale walio katika Yudea waanze kukimbilia milimani. Mwacheni mtu aliye juu ya paa ya nyumba asiteremke, wala asiingie ndani kuchukua kitu chochote kutoka nyumbani mwake; na mwacheni mtu aliye katika shamba asirudi kwa mambo yaliyo nyuma kuchukua vazi lake la nje. Ole wao wanawake wenye mimba na wale wanaonyonyesha kitoto kichanga katika siku hizo! Fulizeni kusali kwamba isipate kutukia wakati wa majira ya baridi kali.”—Marko 13:14-18.
-
-
“Mwacheni Msomaji Atumie Ufahamu”Mnara wa Mlinzi—1999 | Mei 1
-
-
22. Huenda kutii kwetu shauri la Yesu kuhusu kukimbilia milimani kukahusisha nini?
22 Kwa sasa, hatuwezi kujua mambo yote kuhusu dhiki kubwa, lakini twaweza kukata kauli ifaavyo kwamba kule kukimbia ambako Yesu alizungumzia hakutahusu kukimbilia mahali halisi. Tayari sasa watu wa Mungu wanapatikana tufeni pote, karibu kila mahali duniani. Hata hivyo, twaweza kuwa na uhakika kwamba wakati kukimbia kutakapohitajika, itabidi Wakristo waendelee kudumisha tofauti iliyo wazi baina yao na matengenezo ya dini zisizo za kweli. Pia, ni jambo lenye maana kwamba Yesu alionya kuhusu mtu kurudi nyumbani mwake ili kuchukua nguo na bidhaa nyingine. (Mathayo 24:17, 18) Kwa hiyo, huenda majaribu yako mbele kuhusiana na jinsi tunavyoziona mali za kimwili; je, hivyo ndivyo vitu muhimu zaidi, au je, ule wokovu utakaowajia wale wote walio upande wa Mungu ni wa muhimu zaidi? Naam, huenda kukimbia kwetu kukahusisha magumu fulani na hasara. Itatubidi tuwe tayari kufanya lolote lihitajiwalo, kama walivyofanya Wakristo wenzetu wa karne ya kwanza, ambao walikimbia kutoka Yudea hadi Perea, iliyo ng’ambo ya Yordani.
-