Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mwacheni Msomaji Atumie Ufahamu”
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Mei 1
    • 18, 19. Ni sababu zipi zimetolewa kuonyesha kwamba “kukimbilia milimani” hakutamaanisha kubadili dini?

      18 Baada ya kutabiri kuhusu ‘kitu chenye kuchukiza sana kikisimama katika mahali patakatifu,’ Yesu aliwaonya wenye ufahamu wachukue hatua. Je, alimaanisha kwamba kufikia wakati huo wa mwisho—wakati ambapo “kitu chenye kuchukiza sana” “kikiwa kimesimama katika mahali patakatifu”—watu wengi wataikimbia dini isiyo ya kweli na kujiunga na ibada ya kweli? Sivyo. Ufikirie utimizo wa kwanza. Yesu alisema hivi: “Waacheni wale walio katika Yudea waanze kukimbilia milimani. Mwacheni mtu aliye juu ya paa ya nyumba asiteremke, wala asiingie ndani kuchukua kitu chochote kutoka nyumbani mwake; na mwacheni mtu aliye katika shamba asirudi kwa mambo yaliyo nyuma kuchukua vazi lake la nje. Ole wao wanawake wenye mimba na wale wanaonyonyesha kitoto kichanga katika siku hizo! Fulizeni kusali kwamba isipate kutukia wakati wa majira ya baridi kali.”—Marko 13:14-18.

  • “Mwacheni Msomaji Atumie Ufahamu”
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Mei 1
    • 23, 24. (a) Ni mahali gani pekee tutakapopata ulinzi? (b) Onyo la Yesu kuhusu ‘kitu chenye kuchukiza sana kikiwa kimesimama katika mahali patakatifu’ lapasa kutuathirije?

      23 Ni lazima tuwe na uhakika kwamba Yehova, na tengenezo lake lililo kama mlima, anaendelea kuwa kimbilio letu. (2 Samweli 22:2, 3; Zaburi 18:2; Danieli 2:35, 44) Katika yeye tutapata ulinzi! Hatutaiga umati wa wanadamu utakaokimbilia “mapango” na kujificha katika “matungamo-miamba ya milima”—matengenezo na mashirika ya kibinadamu ambayo huenda yakabakia kwa wakati mfupi sana baada ya Babiloni Mkubwa kufanywa ukiwa. (Ufunuo 6:15; 18:9-11) Ni kweli kwamba huenda nyakati zikawa ngumu—kama vile inavyoelekea zilikuwa kwa wanawake wajawazito mwaka wa 66 W.K. waliokimbia kutoka Yudea au wowote waliolazimika kusafiri katika hali yenye baridi na mvua. Lakini twaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu atafanya kuokoka kuwezekane. Acheni, hata sasa, tuimarishe tumaini letu kwa Yehova na kwa Mwana wake, ambaye sasa anatawala akiwa Mfalme wa Ufalme.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki