-
Yosefu wa Arimathea Achukua MsimamoMnara wa Mlinzi (Funzo)—2017 | Oktoba
-
-
YOSEFU WA ARIMATHEA hakujua alipata wapi ujasiri wa kwenda mbele ya gavana Mroma Pontio Pilato. Gavana huyo alijulikana kuwa mtu mkaidi sana. Hata hivyo, ili Yesu azikwe kwa njia ya heshima, lazima mtu fulani angehitaji kwenda kwa Pilato na kumwomba mwili wa Yesu. Yosefu alipokutana uso kwa uso na Pilato, mambo hayakuwa magumu kama ambavyo huenda alitarajia. Baada ya kuhakikisha kutoka kwa ofisa mmoja kwamba Yesu alikuwa amekufa, Pilato alikubali ombi la Yosefu. Kisha Yosefu akiwa bado mwenye huzuni nyingi akarudi haraka mahali ambapo Yesu aliuawa.—Marko 15:42-45.
-
-
Yosefu wa Arimathea Achukua MsimamoMnara wa Mlinzi (Funzo)—2017 | Oktoba
-
-
ALIKUWA MSHIRIKI WA SANHEDRINI
Injili ya Marko iliyoongozwa na roho ya Mungu inamtaja Yosefu kuwa “mshiriki wa Baraza mwenye kusifika.” Muktadha wa andiko hilo unaonyesha kwamba Baraza hilo lilikuwa Sanhedrini—mahakama kuu ya Wayahudi na baraza kuu la usimamizi. (Marko 15:1, 43) Hivyo, Yosefu alikuwa mmoja wa viongozi wa Wayahudi, na ndiyo sababu angeweza kwenda kuzungumza na gavana Mroma. Kwa hiyo, haishangazi kwamba Yosefu alikuwa tajiri pia.—Mt. 27:57.
Je, una ujasiri wa kumkiri Yesu kuwa Mfalme wako?
Kwa ujumla, Sanhedrini ilimchukia Yesu. Washiriki wake walipanga njama ya kumuua. Hata hivyo, Yosefu anatajwa kuwa “mtu mwema na mwadilifu.” (Luka 23:50) Tofauti na wengi wa washiriki wenzake wa Sanhedrini, Yosefu alikuwa mnyoofu, mwenye maadili, na alijitahidi kutii amri za Mungu. Alikuwa pia “akiungojea ufalme wa Mungu,” jambo linaloweza kutusaidia kuelewa kwa nini alikuwa mwanafunzi wa Yesu. (Marko 15:43; Mt. 27:57) Inawezekana kwamba alivutiwa na ujumbe wa Yesu kwa sababu alipenda sana kweli na haki.
-
-
Yosefu wa Arimathea Achukua MsimamoMnara wa Mlinzi (Funzo)—2017 | Oktoba
-
-
ASHINDA WOGA
Kufikia wakati ambapo Yesu alikufa, ni wazi kwamba Yosefu alikuwa ameshinda hisia za woga alizokuwa nazo, naye akaamua kushirikiana na wafuasi wa Yesu. Tunajua hivyo kwa kuwa andiko la Marko 15:43 linasema hivi: “Akajipa moyo kuingia mbele ya Pilato na kuomba apewe mwili wa Yesu.”
-