-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—1990 | Machi 15
-
-
Maswali Kutoka kwa Wasomaji
◼ Je! yatupasa tukate shauri kutokana na Mathayo 7:13, 14 na Luka 13:24 kwamba hata katika ufufuo, wanadamu walio wengi watakataa ibada ya kweli?
Sivyo, mistari hii haiungi mkono kukata shauri jinsi hiyo. Bali, yahusu hasa kupata uhai katika Ufalme wa kimbingu.
-
-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—1990 | Machi 15
-
-
Maana ya Luka 13:24 yafanana na hiyo, kama ionyeshwavyo na habari zenye kuzunguka. Yesu alitoa vielezi viwili juu ya “ufalme wa Mungu.” Baadaye, aliulizwa hivi: “Je! Bwana, watu wanaookolewa ni wachache?” Yesu alijibu: “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.” “Wengi” yarejezea watu walioomba sana waruhusiwe kuingia baada ya mlango kufungwa na kutiwa kufuli. Hawa walikuwa “wafanyaji wa udhalimu” ambao hawakustahili kuwa na ‘Abrahamu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu.’ “Wengi” hao walikuwa wamefikiri wangekuwa wa kwanza “katika ufalme wa Mungu,” lakini kwa kweli wangekuwa ndio wa mwisho, kwa wazi ikimaanisha kwamba hawangekuwa humo hata kidogo.—Luka 13:18-30.
Habari zenye kuzunguka zaonyesha kwamba Yesu alikuwa akishughulikia kuingia ndani ya Ufalme wa kimbingu wa Mungu. Viongozi wa Kiyahudi huko nyuma walikuwa wameonea shangwe cheo chenye pendeleo, wakiwa na fursa ya kuwa na Neno la Mungu. Walihisi kwamba walikuwa matajiri kiroho na waadilifu machoni pa Mungu, tofauti na watu wa kawaida, ambao wao waliwadharau. (Yohana 9:24-34) Hata hivyo, Yesu alisema kwamba wakusanya kodi na makahaba waliokubali ujumbe wake na kutubu wangeweza kuwa na kibali cha Mungu.—Linganisha Mathayo 21:23-32; Luka 16:14-31.
Watu wa kawaida waliokuja kuwa wanafunzi wa Yesu walikuwa katika mstari wa kukubaliwa kuwa wana wa kiroho wakati wito wa kimbingu ulipofunguka wazi kwenye Pentekoste 33 W.K. (Waebrania 10:19, 20) Ingawa umati wa watu wengi sana ulisikia Yesu, wale waliomkubali na baadaye wakapata tumaini la kimbingu walikuwa wachache. Lakini kundi dogo la wanadamu waliozaliwa kwa roho wenye kupokea thawabu hiyo wangeweza kulinganishwa na Yakobo akiegemea mezani akiwa mbinguni pamoja na Yehova (Abrahamu Mkubwa Zaidi) na Mwana wake (aliyefananishwa na Isaka). Kwa uhakika hilo ni jambo lililostahiki kujitahidi kisulubu, lakini walio wengi wa wale waliosikia Yesu hawakufanya hivyo.
Kwa hiyo, twaweza kuona kutokana na habari zenye kuzunguka vituko vyote viwili kwamba maelezo ya Yesu (juu ya kuwa kwa wachache katika barabara iliyosonga inayoongoza kwenye uhai na kuokolewa kwao) yalihusu hasa kuwa na kibali cha Mungu wakati huo ambapo Yeye alikuwa akitoa tumaini la uhai wa kimbingu. Waliosikia ujumbe wa ukweli na kujifunza yaliyotakwa na kuitikia wakathibitika kuwa waaminifu ni wachache kwa ulinganisho.— Mathayo 22:14; 24:13; Yohana 6:60-66.
-