Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Iweni na Upendo Miongoni Mwenu Wenyewe’
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Februari 1
    • 5, 6. (a) Yesu alisimulia vielezi gani viwili vifupi? (b) Vielezi hivyo vinaonyesha nini kuhusu Yehova?

      5 Ili kuwafundisha wasikilizaji wake jinsi Yehova anavyowaona wale ambao wamepoteza mwelekeo, Yesu alisimulia vielezi viwili vifupi. Kielezi kimoja kilihusu mchungaji. Yesu alisema: “Ni mtu gani kati yenu mwenye kondoo mia, apotezapo mmoja wao, hataacha nyuma wale tisini na tisa nyikani na kwenda kumtafuta aliyepotea mpaka ampate? Na akiisha kumpata humweka juu ya mabega yake na kushangilia. Naye afikapo nyumbani huita marafiki wake na majirani wake pamoja, akiwaambia, ‘Shangilieni pamoja nami, kwa sababu nimempata kondoo wangu aliyekuwa amepotea.’ Mimi nawaambia nyinyi kwamba ndivyo kutakuwa na shangwe zaidi mbinguni juu ya mtenda-dhambi mmoja atubuye kuliko juu ya waadilifu tisini na tisa wasio na uhitaji wa toba.”—Luka 15:4-7.

  • ‘Iweni na Upendo Miongoni Mwenu Wenyewe’
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Februari 1
    • Kilipotea Lakini Kilithaminiwa

      8. (a) Mchungaji na mwanamke walihisije vitu vyao vilipopotea? (b) Tunajifunza nini kutokana na jinsi walivyohisi kuhusu vitu vilivyopotea?

      8 Katika vielezi vyote viwili, kitu fulani kilipotea, lakini ona jinsi wenye vitu hivyo walivyohisi. Mchungaji hakusema: ‘Kondoo mmoja ana faida gani, je, sina kondoo 99? Simhitaji kondoo huyo.’ Mwanamke huyo hakusema: ‘Kwa nini nihangaikie sarafu moja? Zile tisa nilizo nazo zanitosha.’ Badala ya kusema hivyo, mchungaji alimtafuta kondoo aliyepotea kana kwamba alikuwa na kondoo huyo mmoja tu. Naye mwanamke huyo aliona kwamba amepata hasara kwa kupoteza sarafu moja kana kwamba hakuwa na sarafu nyingine. Katika visa vyote viwili, wenye vitu hivyo vilivyopotea waliviona kuwa vyenye thamani. Tunajifunza nini?

      9. Ni nini kinachoonyeshwa na hangaiko la mchungaji na mwanamke?

      9 Ona jinsi Yesu alivyomalizia vielezi vyote viwili: “Ndivyo kutakuwa na shangwe zaidi mbinguni juu ya mtenda-dhambi mmoja atubuye” na “ndivyo shangwe hutokea miongoni mwa malaika za Mungu juu ya mtenda-dhambi mmoja atubuye.” Kwa hiyo, hangaiko lililoonyeshwa na mchungaji na mwanamke huyo linatufundisha kwa kiwango kidogo jinsi Yehova na viumbe wake walio mbinguni wanavyohisi. Kwa hiyo, wale ambao wamepoteza mwelekeo na kuacha kushirikiana na watu wa Mungu ni wenye thamani machoni pa Yehova kama vile vitu vilivyopotea vilivyokuwa na thamani kwa mchungaji na mwanamke. (Yeremia 31:3) Huenda watu hao wakawa dhaifu kiroho, lakini huenda wasiwe waasi. Licha ya udhaifu wao, huenda kwa kadiri fulani wakawa wanajitahidi kutimiza matakwa ya Yehova. (Zaburi 119:176; Matendo 15:29) Kwa hiyo, kama ilivyokuwa zamani, Yehova hafanyi haraka ‘kuwatupa usoni pake.’—2 Wafalme 13:23.

      10, 11. (a) Tungependa kuwaonaje wale ambao wameacha kushirikiana na kutaniko? (b) Kulingana na vielezi viwili vya Yesu, tunaweza kuonyeshaje kwamba tunawajali?

      10 Kama Yehova na Yesu, sisi pia tunawajali sana wale walio dhaifu na ambao hawashirikiani na kutaniko la Kikristo. (Ezekieli 34:16; Luka 19:10) Tunamwona mtu aliye dhaifu kiroho kama kondoo aliyepotea—si mtu asiyeweza kusaidiwa. Hatusemi: ‘Kwa nini tujishughulishe na mtu aliye dhaifu? Kutaniko linaendelea vizuri bila yeye.’ Badala yake, tunawaona wale ambao wameacha njia na wanaotaka kurudi kama Yehova anavyowaona—kuwa wenye thamani.

  • ‘Iweni na Upendo Miongoni Mwenu Wenyewe’
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Februari 1
    • Pendezwa Nao

      12. Maneno ‘kwenda kumtafuta aliyepotea’ yanaonyesha nini kuhusu mtazamo wa mchungaji?

      12 Katika kielezi cha kwanza kati ya vielezi hivyo viwili, Yesu anasema kwamba mchungaji ‘atakwenda kumtafuta aliyepotea.’ Mchungaji anaonyesha upendezi na kujitahidi kutafuta kondoo aliyepotea. Mchungaji huyo hazuiwi na magumu, hatari, wala umbali. Badala yake anaendelea na jitihada yake “mpaka ampate.”—Luka 15:4.

      13. Wanaume wa kale wenye imani walichukua hatua gani kuelekea walio dhaifu, nasi tunawezaje kuiga mifano hiyo ya Biblia?

      13 Vivyo hivyo, ili kusaidia mtu anayehitaji kutiwa moyo mara nyingi mwenye nguvu anapaswa kuonyesha upendezi. Wanaume waaminifu wa kale walifahamu jambo hilo. Kwa mfano, Yonathani, mwana wa Mfalme Sauli alipotambua kwamba rafiki yake wa chanda na pete, Daudi, alihitaji kutiwa moyo, Yonathani “akainuka akamwendea Daudi huko Horeshi, akamtia nguvu mkono wake katika Mungu.” (1 Samweli 23:15, 16) Karne kadhaa baadaye, Gavana Nehemia alipoona kwamba baadhi ya ndugu zake Wayahudi walikuwa wamevunjika moyo, yeye pia ‘mara moja alisimama’ na kuwatia moyo ‘wamkumbuke Yehova.’ (Nehemia 4:14, NW) Leo, sisi pia tungependa ‘kusimama—kuonyesha upendezi—kuimarisha walio dhaifu. Lakini ni nani wanaopaswa kufanya hivyo kutanikoni?

      14. Ni nani anayepaswa kusaidia walio dhaifu katika kutaniko la Kikristo?

      14 Wazee Wakristo hasa wana daraka la ‘kutia nguvu mikono iliyo dhaifu na kufanya imara magoti yaliyolegea’ na ‘kuwaambia walio na moyo wa hofu, Jipeni moyo, msiogope.’ (Isaya 35:3, 4; 1 Petro 5:1, 2) Hata hivyo, shauri la Paulo juu ya ‘kusema kwa kuliwaza nafsi zilizoshuka moyo’ na ‘kutegemeza walio dhaifu’ halikutolewa kwa wazee peke yao. Badala yake, maneno ya Paulo yalihusu ‘kutaniko lote la Wathesalonike.’ (1 Wathesalonike 1:1; 5:14) Kwa hiyo Wakristo wote wana daraka la kusaidia walio dhaifu. Kama yule mchungaji katika kielezi cha Yesu, kila Mkristo anapaswa kuchochewa “kwenda kumtafuta aliyepotea.” Bila shaka, tunaweza kutoa msaada huo kwa njia inayofaa kwa kushirikiana na wazee. Je, unaweza kufanya jambo fulani kusaidia mtu aliye dhaifu katika kutaniko lenu?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki