-
‘Iweni na Upendo Miongoni Mwenu Wenyewe’Mnara wa Mlinzi—2003 | Februari 1
-
-
6 Kielezi cha pili kilihusu mwanamke fulani. Yesu alisema: “Ni mwanamke gani mwenye sarafu za drakma kumi, ikiwa apoteza sarafu moja ya drakma, asiyewasha taa na kufagia nyumba yake na kutafuta kwa uangalifu mpaka aipate? Naye akiisha kuipata huwaita wanawake walio marafiki wake na majirani pamoja, akisema, ‘Shangilieni pamoja nami, kwa sababu nimeipata sarafu ya drakma niliyoipoteza.’ Hivyo, mimi nawaambia nyinyi, ndivyo shangwe hutokea miongoni mwa malaika za Mungu juu ya mtenda-dhambi mmoja atubuye.”—Luka 15:8-10.
-
-
‘Iweni na Upendo Miongoni Mwenu Wenyewe’Mnara wa Mlinzi—2003 | Februari 1
-
-
Kilipotea Lakini Kilithaminiwa
8. (a) Mchungaji na mwanamke walihisije vitu vyao vilipopotea? (b) Tunajifunza nini kutokana na jinsi walivyohisi kuhusu vitu vilivyopotea?
8 Katika vielezi vyote viwili, kitu fulani kilipotea, lakini ona jinsi wenye vitu hivyo walivyohisi. Mchungaji hakusema: ‘Kondoo mmoja ana faida gani, je, sina kondoo 99? Simhitaji kondoo huyo.’ Mwanamke huyo hakusema: ‘Kwa nini nihangaikie sarafu moja? Zile tisa nilizo nazo zanitosha.’ Badala ya kusema hivyo, mchungaji alimtafuta kondoo aliyepotea kana kwamba alikuwa na kondoo huyo mmoja tu. Naye mwanamke huyo aliona kwamba amepata hasara kwa kupoteza sarafu moja kana kwamba hakuwa na sarafu nyingine. Katika visa vyote viwili, wenye vitu hivyo vilivyopotea waliviona kuwa vyenye thamani. Tunajifunza nini?
-
-
‘Iweni na Upendo Miongoni Mwenu Wenyewe’Mnara wa Mlinzi—2003 | Februari 1
-
-
9. Ni nini kinachoonyeshwa na hangaiko la mchungaji na mwanamke?
9 Ona jinsi Yesu alivyomalizia vielezi vyote viwili: “Ndivyo kutakuwa na shangwe zaidi mbinguni juu ya mtenda-dhambi mmoja atubuye” na “ndivyo shangwe hutokea miongoni mwa malaika za Mungu juu ya mtenda-dhambi mmoja atubuye.” Kwa hiyo, hangaiko lililoonyeshwa na mchungaji na mwanamke huyo linatufundisha kwa kiwango kidogo jinsi Yehova na viumbe wake walio mbinguni wanavyohisi. Kwa hiyo, wale ambao wamepoteza mwelekeo na kuacha kushirikiana na watu wa Mungu ni wenye thamani machoni pa Yehova kama vile vitu vilivyopotea vilivyokuwa na thamani kwa mchungaji na mwanamke. (Yeremia 31:3) Huenda watu hao wakawa dhaifu kiroho, lakini huenda wasiwe waasi. Licha ya udhaifu wao, huenda kwa kadiri fulani wakawa wanajitahidi kutimiza matakwa ya Yehova. (Zaburi 119:176; Matendo 15:29) Kwa hiyo, kama ilivyokuwa zamani, Yehova hafanyi haraka ‘kuwatupa usoni pake.’—2 Wafalme 13:23.
10, 11. (a) Tungependa kuwaonaje wale ambao wameacha kushirikiana na kutaniko? (b) Kulingana na vielezi viwili vya Yesu, tunaweza kuonyeshaje kwamba tunawajali?
10 Kama Yehova na Yesu, sisi pia tunawajali sana wale walio dhaifu na ambao hawashirikiani na kutaniko la Kikristo. (Ezekieli 34:16; Luka 19:10) Tunamwona mtu aliye dhaifu kiroho kama kondoo aliyepotea—si mtu asiyeweza kusaidiwa. Hatusemi: ‘Kwa nini tujishughulishe na mtu aliye dhaifu? Kutaniko linaendelea vizuri bila yeye.’ Badala yake, tunawaona wale ambao wameacha njia na wanaotaka kurudi kama Yehova anavyowaona—kuwa wenye thamani.
-