-
“Yehova, Mungu Mwenye Rehema na Neema”Mnara wa Mlinzi—1998 | Oktoba 1
-
-
9, 10. (a) Mwana mpotevu alipatwa na badiliko gani la hali, naye alitendaje kulihusu? (b) Toa kielezi cha jinsi ambavyo wengine leo ambao huacha ibada ya kweli hupatwa na hali mbaya sawa na iliyompata mwana mpotevu.
9 “Alipokuwa ametumia kila kitu, njaa kali sana ilitokea kotekote katika nchi hiyo, naye akaanza kuwa katika uhitaji. Hata alienda na kujiambatanisha mwenyewe kwa mmoja wa raia wa nchi hiyo, naye akamtuma aingie katika mashamba yake ili achunge mifugo ya nguruwe. Naye alikuwa na kawaida ya kutamani kushibishwa kwa matumba ya mkarobu ambayo hao nguruwe walikuwa wakila, na hakuna yeyote aliyekuwa akimpa kitu chochote.”—Luka 15:14-16.
-
-
“Yehova, Mungu Mwenye Rehema na Neema”Mnara wa Mlinzi—1998 | Oktoba 1
-
-
11. Tatizo la mwana mpotevu lilifanywaje kuwa baya zaidi, na wengine leo wametambuaje kwamba vivutio vya ulimwengu ni “udanganyo mtupu”?
11 Tatizo la mwana mpotevu lilifanywa kuwa baya zaidi na uhakika wa kwamba “hakuna yeyote aliyekuwa akimpa kitu chochote.” Marafiki aliokuwa amepata karibuni walikuwa wapi? Kwa vile sasa alikuwa hana hata ndururu, kwao alikuwa kama “kitu cha kuchukiwa.” (Mithali 14:20, NW) Hali kadhalika, watu wengi leo ambao hupotea njia na kuacha imani hutambua kwamba vivutio na maoni ya ulimwengu huu ni sawa na “udanganyo mtupu.” (Wakolosai 2:8) “Bila mwongozo wa Yehova, nilipatwa na maumivu na huzuni nyingi,” asema mwanamke mmoja kijana ambaye aliacha tengenezo la Mungu kwa muda fulani. “Nilijaribu kujipatanisha na ulimwengu, lakini kwa sababu kwa kweli nilikuwa tofauti na wengine, walinikataa. Nilijihisi kama mtoto aliyepotea ambaye alihitaji baba wa kumwongoza. Ndipo nilipotambua kwamba nilimhitaji Yehova. Sikutaka kamwe kuishi bila kumtegemea.” Mwana mpotevu katika kielezi cha Yesu alitambua jambo lililo sawa na hilo.
-