-
Je! Wakati Mmoja Wewe Ulishirikiana na Tengenezo la Yehova?Mnara wa Mlinzi—1988 | Januari 15
-
-
Lakini ni upokezi wa namna gani ambao angeweza kutazamia kutoka kwa baba yake kama angerudi sasa? Ingeweza kuwa vigumu kwake kutazamia kusalimiwa kwa uchangamfu au hata kuruhusiwa aingie ndani ya nyumba ile baada ya kuwa ametumia vibaya kwa njia ya aibu sana fadhili za baba yake. Hata hivyo, hisia ya kina kirefu ilitawala akili na moyo wake: Lazima aende nyumbani.
Mwanamume kijana huyo kumbe hakuelewa vizuri sana hisia za baba yake kumhusu yeye! Ni kishtushi kikubwa kama nini kilichomngoja yeye alipokuwa akikaribia maskani yake ya zamani! Kwa kweli, “huku yeye akiwa bado umbali mrefu kutoka hapo, baba yake alipata kumwona na akasukumwa na sikitikio, na yeye akapiga mbio na kuanguka juu ya shingo yake na kumbusu yeye kwa wororo mwingi.”—Luka 15:20, NW.
Kama yule mwana mpotevu, je! wewe umeacha maskani yako ya kiroho? Je! wewe umepeperuka kutoka kwa Baba yako, Yehova, na tengenezo lake? Je! sasa pia unatamani ‘kuja nyumbani’?
-
-
Je! Wakati Mmoja Wewe Ulishirikiana na Tengenezo la Yehova?Mnara wa Mlinzi—1988 | Januari 15
-
-
Lakini kundi la Kikristo limekuwa haliketi tu likingojea kukaribisha watu hao ikiwa na iwapo wao wataamua ‘kuja nyumbani.’ Katika kielezi cha Yesu, yule baba alipiga mbio nje kulaki mwana wake wakati “yeye alipokuwa bado umbali mrefu kutoka hapo.” Vivyo hivyo, Mashahidi wa Yehova wanaufikiria kuwa wajibu wa kibinafsi kutafuta wale ambao wakati mmoja walishiriki, na kusaidia hao warudi ndani ya tengenezo la Yehova.
-