-
Wakati Mwana Mpotevu AnapopatwaMnara wa Mlinzi—1989 | Februari 15
-
-
Kwa wakati huo, ‘mwana mkubwa wa baba alikuwako shambani.’ Ona kama unaweza kutambua yeye anawakilisha nani kwa kusikiliza sehemu iliyobaki ya hadithi. Yesu anasema hivi juu ya mwana huyo mkubwa: “Alipokuwa akija na kuikaribia nyumba, alisikia sauti ya nyimbo na machezo. Akaita mtumishi mmoja, akamwuliza, Mambo haya, maana yake nini? Akamwambia, Ndugu yako amekuja, na baba yako amemchinja ndama aliyenona, kwa sababu amempata tena, yu mzima. Akakasirika, akakataa kuingia ndani.
“Basi babaye alitoka nje, akamsihi. Akamjibu baba yake, akasema, Tazama, mimi nimekutumikia miaka mingapi hii, wala sijakosa amri yako wakati wo wote, lakini hujanipa mimi mwana-mbuzi, nifanye furaha na rafiki zangu; lakini, alipokuja huyu mwana wako aliyekula vitu vyako pamoja na makahaba, umemchinjia yeye ndama aliyenona.”
Ni nani, akiwa kama yule mwana mkubwa, amekuwa akichambua-chambua rehema na fikira wanazopewa watenda dhambi? Je! si waandishi na Mafarisayo? Kwa kuwa kilichofanya kielezi hiki kitolewe ni uchambuzi wao juu ya Yesu kwa sababu ya yeye kukaribisha watenda dhambi, kwa uwazi ni lazima iwe wao ndio waliowakilishwa na yule mwana mkubwa.
-
-
Wakati Mwana Mpotevu AnapopatwaMnara wa Mlinzi—1989 | Februari 15
-
-
Lakini katika nyakati za ki-siku-hizi wana hao wawili wanawakilisha nani? Lazima iwe ni wale ambao wamepata kujua mambo ya kutosha juu ya makusudi ya Yehova hata wawe na msingi wa kuingia katika uhusiano pamoja naye. Mwana mkubwa anawakilisha washiriki fulani wa “kundi dogo,” au “kanisa [kundi, NW] la wazaliwa wa kwanza walioandikwa mbinguni.” Hao walichagua kufuata mwelekeo unaofanana na ule wa mwana mkubwa. Hawakutaka kukaribisha jamii ya kidunia, “kondoo wengine,” wakihisi kwamba hao walikuwa wakifanya wao waache kujulikana kwa umashuhuri mwingi kama zamani.
-