Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutafuta Utajiri wa Kweli
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2017 | Julai
    • 4, 5. (a) Msimamizi-nyumba katika mfano wa Yesu alijikuta katika hali gani? (b) Yesu aliwapa wafuasi wake himizo gani?

      4 Soma Luka 16:​1-9. Mfano wa Yesu kuhusu msimamizi-nyumba asiye mwadilifu unafanya tufikiri. Baada ya kushtakiwa kwamba alitumia mali vibaya, msimamizi-nyumba huyo alitenda kwa “hekima inayotumika” ‘kujifanyia rafiki’ ambao wangemsaidia atakapopoteza usimamizi-nyumba.a Bila shaka, Yesu hakuwa akiwatia moyo wanafunzi wake watende kwa ukosefu wa uadilifu ili wafanikiwe katika ulimwengu huu. Alisema kuwa tabia hiyo ni ya “wana wa mfumo huu wa mambo,” lakini alitumia mfano huo kufundisha somo fulani.

      5 Yesu alijua kuwa kama msimamizi-nyumba aliyejikuta katika hali ngumu, wafuasi wengi wa Yesu wangehitaji kujiruzuku katika ulimwengu huu wa kibiashara usio na haki. Kwa hiyo, anawahimiza hivi: “Jifanyieni rafiki kupitia mali zisizo za uadilifu, ili, zitakapopunguka [Yehova na Yesu] wawapokee ninyi katika makao ya milele.” Tunaweza kujifunza nini kutokana na shauri la Yesu?

      6. Tunajuaje kwamba ulimwengu wa sasa wa kibiashara haukuwa sehemu ya kusudi la Mungu?

      6 Ingawa Yesu haelezi kwa nini aliita mali hizo “mali zisizo za uadilifu,” Biblia inaonyesha wazi kwamba biashara haikuwa sehemu ya kusudi la Mungu. Yehova aliwaandalia Adamu na Hawa mahitaji yao kwa wingi katika shamba la Edeni. (Mwa. 2:​15, 16) Baadaye, roho takatifu ilipotenda juu ya kutaniko la watiwa mafuta la karne ya kwanza, “hakuna hata mmoja aliyekuwa akisema kwamba chochote kati ya vitu vilivyokuwa mali yake kilikuwa chake mwenyewe; bali walikuwa na vitu vyote kwa ushirika.” (Mdo. 4:​32) Nabii Isaya alizungumzia wakati ambapo wanadamu wote wangefurahia kikamili rasilimali za dunia. (Isa. 25:​6-9; 65:​21, 22) Lakini kabla ya wakati huo, wafuasi wa Yesu wangehitaji “hekima inayotumika” ili kujiruzuku kwa kutumia “mali zisizo za uadilifu” za ulimwengu wa sasa huku wakijitahidi kumpendeza Mungu.

  • Kutafuta Utajiri wa Kweli
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2017 | Julai
    • 7. Tunapata shauri gani katika Luka 16:​10-​13?

      7 Soma Luka 16:​10-​13. Msimamizi-nyumba katika mfano wa Yesu alijifanyia rafiki kwa faida za kibinafsi. Hata hivyo, Yesu aliwahimiza wafuasi wake wajifanyie rafiki mbinguni kwa sababu zisizo za ubinafsi. Baada ya mfano huo, mistari inayofuata inahusianisha “mali zisizo za uadilifu” na kuwa mwaminifu kwa Mungu. Yesu alimaanisha kwamba tunaweza “[kujionyesha] wenyewe kuwa waaminifu” kupitia jinsi tunavyotumia mali hizo baada ya kuzipata. Jinsi gani?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki