-
Panga Mapema—Tumia Hekima InayotumikaYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Yesu hakubaliani na njia ambayo yule msimamizi alitumia, wala haungi mkono kutumia udanganyifu katika biashara. Basi, anafundisha somo gani? Anawahimiza hivi wanafunzi: “Jifanyieni marafiki kupitia mali zisizo za uadilifu, ili zitakapokwisha wawapokee katika makao ya milele.” (Luka 16:9) Naam, hapa kuna somo kuhusu kupanga mapema na kutumia hekima inayotumika. Watumishi wa Mungu, yaani, “wana wa nuru,” wanapaswa kutumia mali zao za kimwili kwa njia ya hekima, wakifikiria kuhusu wakati ujao wa milele.
Yehova na Yesu ndio tu wanaoweza kumpokea mtu katika Ufalme wa mbinguni au Paradiso duniani chini ya Ufalme huo. Tunapaswa kujitahidi kusitawisha urafiki pamoja nao kwa kutumia mali zetu za kimwili kuunga mkono kazi ya Ufalme. Kwa njia hiyo, wakati wetu ujao wa milele utakuwa salama wakati dhahabu, fedha, na utajiri mwingine wa kimwili utakapokwisha au kuangamia.
-
-
Panga Mapema—Tumia Hekima InayotumikaYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Yesu anawaonyesha wanafunzi wake kwamba watadaiwa mengi ikiwa wanataka kupokelewa “katika makao ya milele.” Mtu hawezi kuwa mtumishi wa kweli wa Yehova na wakati uleule awe mtumwa wa utajiri wa kimwili usio wa uadilifu. Yesu anamalizia kwa kusema: “Hakuna mtumishi anayeweza kuwatumikia mabwana wawili, kwa maana atamchukia mmoja na kumpenda mwingine, au atashikamana na mmoja na kumdharau mwingine. Hamwezi kuwa watumwa wa Mungu na wa Utajiri.”—Luka 16:9, 13.
-