-
Tajiri na Lazaro Wapatwa na BadilikoMnara wa Mlinzi—1989 | Aprili 1
-
-
“Halafu,” Yesu anasema, “yule masikini alikufa, akachukuliwa na malaika katika kifua chake Abrahamu; yule tajiri alikufa vilevile, akazikwa. Katika Hadeze akiwa katika azabu [mateso, UV], akanyanyua macho yake, akaona Abrahamu mbali na Lazaro katika kifua chake.”
Kwa kuwa tajiri na Lazaro si watu halisi bali wanafananisha jamii za watu, ni jambo la kiakili kuchukua vifo vyao kuwa vya ufananisho. Vifo vyao vinafananisha au kuwakilisha nini?
Yesu amemaliza sasa tu kuelekeza kwenye badiliko la hali kwa kusema kwamba ‘Torati na manabii zilikuwa hata Yoane Mbatizaji, lakini tangu wakati huo ufalme wa Mungu unahubiriwa.’ Kwa sababu hiyo, Yohana na Yesu Kristo wafanyapo kuhubiri kwao ndipo wote wawili tajiri na Lazaro wanapokufa kuhusu hali zao za kwanza.
Wale walio wa jamii ya Lazaro mnyenyekevu mwenye kutubu wanakufa kuhusu hali yao ya kwanza ya kunyimwa uhitaji wa kiroho na wanakuja ndani ya cheo cha upendeleo wa kimungu. Ijapokuwa mapema kidogo walitegemea viongozi wa kidini kwa kiasi chochote kidogo kilichoanguka kutoka meza ya kiroho, sasa kweli za Kimaandiko zinazotolewa na Yesu zinajaza mahitaji yao. Hivyo wanaletwa ndani ya kifua, au cheo chenye upendeleo, cha Abrahamu Mkubwa Zaidi, Yehova Mungu.
Kwa upande mwingine, wale wanaojumlika kuwa jamii ya tajiri wanakuja chini ya ukosefu wa upendeleo wa kimungu kwa sababu ya kukataa-kataa ujumbe wa Ufalme uliofundishwa na Yesu. Kwa njia hiyo wanakufa kuhusu cheo walichokuwa nacho cha kuonekana kama wenye upendeleo. Kwa uhakika, wananenwa kama kwamba wamo katika mteseko-teseko wa kitamathali. Sikiliza wakati tajiri anaponena:
-
-
Tajiri na Lazaro Wapatwa na BadilikoMnara wa Mlinzi—1989 | Aprili 1
-
-
Ni haki na inafaa kama nini badiliko hilo la kutazamisha litukie kati ya jamii ya Lazaro na jamii ya tajiri! Badiliko hilo la hali linatimizwa miezi michache baadaye kwenye Pentekoste 33 W.K., wakati nafasi ya agano la zamani la Sheria (Torati) inapochukuliwa na agano jipya. Ndipo inapoonekana wazi kwa njia isiyoweza kukosewa kwamba wanafunzi wanapendelewa na Mungu, wala si Mafarisayo na viongozi wengine wa kidini. Kwa hiyo “shimo kubwa” linalotenganisha tajiri na wanafunzi wa Yesu linawakilisha hukumu ya Mungu isiyobadilika, ya uadilifu.
-