-
Watu Kumi wenye Ukoma Waponywa—Mmoja AshukuruYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Tisa kati ya watu hao wenye ukoma waliotakaswa wanaendelea na safari yao. Mmoja hafanyi hivyo. Mwanamume huyo, Msamaria, anarudi kumtafuta Yesu. Kwa nini? Anathamini sana jambo ambalo Yesu amemfanyia. Mtu huyo aliyekuwa na ukoma ‘anamtukuza Mungu kwa sauti kubwa,’ akitambua kwamba kwa kweli Mungu ndiye amemponya. (Luka 17:15) Anapompata Yesu, anaanguka mbele yake, na kumshukuru.
-
-
Watu Kumi wenye Ukoma Waponywa—Mmoja AshukuruYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Kwa kuwaponya watu hao kumi wenye ukoma, Yesu anaonyesha kwamba anaungwa mkono na Yehova Mungu. Kwa sasa mmoja kati ya wale kumi si kwamba ameponywa kupitia matendo ya Yesu tu, bali pia huenda yuko kwenye njia ya uzima. Hatuishi wakati ambao Mungu anamtumia Yesu kufanya miujiza kama hiyo. Hata hivyo, tukiwa na imani katika Yesu, tunaweza kuwa kwenye njia ya uzima—uzima wa milele. Je, tunaonyesha kwamba tuna shukrani kama Msamaria huyo alivyofanya?
-