-
Je, Ufalme wa Mungu Umo Moyoni Mwako?Maswali ya Biblia Yajibiwa
-
-
Maneno “ufalme wa Mungu umo ndani yenu” yanamaanisha nini?
Tafsiri fulani za Biblia zimewafanya watu fulani wachanganyikiwe kuhusu mahali ambapo Ufalme upo kutokana na jinsi tafsiri hizo zinavyosema katika Luka 17:21. Kwa mfano, tafsiri ya Union Version inasema kwamba “ufalme wa Mungu umo ndani yenu.” Ili kuelewa mstari huo kwa usahihi, tunapaswa kuchunguza muktadha.
Ufalme wa Mungu haukuwa katika mioyo ya watu wakaidi, wauaji, na waliompinga Yesu
Yesu alikuwa akizungumza na Mafarisayo, kikundi cha viongozi wa kidini waliompinga na walioshiriki katika mipango ya kumuua. (Mathayo 12:14; Luka 17:20) Je, inapatana na akili kufikiri kwamba Ufalme ulikuwa hali fulani iliyo ndani ya mioyo yao yenye ukaidi? Yesu aliwaambia: “Ndani mmejaa unafiki na uasi-sheria.”—Mathayo 23:27, 28.
Tafsiri nyingine hufafanua kwa usahihi maneno ya Yesu katika Luka 17:21: “Ufalme wa Mungu uko hapa pamoja nanyi.” (Italiki ni zetu; Contemporary English Version) “Ufalme wa Mungu umo katikati yenu.” (Tafsiri ya Ulimwengu Mpya) Ufalme wa mbinguni ulikuwa “pamoja” au “katikati” ya Mafarisayo, katika maana ya kwamba Yesu, yule aliyeteuliwa na Mungu ili kutawala akiwa Mfalme, alikuwa amesimama mbele yao.—Luka 1:32, 33.
-
-
Je, Ufalme wa Mungu Umo Moyoni Mwako?Maswali ya Biblia Yajibiwa
-
-
a Dini nyingi za Kikristo zinafundisha kwamba Ufalme wa Mungu umo ndani ya mtu, au ndani ya moyo wa mtu. Kwa mfano, nchini Marekani, kanisa fulani la Baptisti (Southern Baptist Convention) lilisema kwamba Ufalme wa Mungu ni sehemu ya “utawala wa Mungu katika moyo na maisha ya mtu mmoja-mmoja.” Vivyo hivyo, katika kitabu chake Jesus of Nazareth, Papa Benedict wa 16 alisema kwamba “Ufalme wa Mungu unakuja kupitia moyo msikivu.”
-