Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je! Upaji Wako Ni Dhabihu?
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Desemba 1
    • “Kila sanduku lilikuwa kwa ajili ya kitu tofauti, ambacho kilionyeshwa na mwandiko katika ulimi wa Kiebrania. La kwanza liliandikwa: Shekeli mpya-mpya; yaani, shekeli zilizowekwa kando kwa ajili ya gharama za mwaka wa sasa. La pili: Shekeli kuukuu; yaani, shekeli zilizowekwa wakfu kwa gharama za mwaka uliotangulia. La tatu: Hua-turturi na njiwa wachanga; pesa ambazo ziliingizwa ndani ya sanduku hilo ndiyo bei iliyolipwa na wale ambao ilikuwa lazima watoe hua-turturi wawili au njiwa wachanga wawili, mmoja akiwa toleo la kuteketeza, yule mwingine akiwa dhabihu kwa ajili ya dhambi. Juu ya lile sanduku la nne iliandikwa hivi: Matoleo ya kuteketeza; pesa hizo zililipia zile gharama za yale matoleo mengine ya kuteketeza. Lile la tano lilikuwa limeandikwa hivi: Kuni, na lilikuwa na zawadi ambazo waaminifu walitoa kwa ajili ya ununuzi wa kuni za madhabahu. Lile la sita: Uvumba (pesa za kununua uvumba). Lile la saba: Kwa ajili ya patakatifu (pesa kwa ajili ya kiti-cha-rehema). Masanduku sita yaliyobaki yaliandikwa hivi: Matoleo ya hiari ya mtu.”

  • Je! Upaji Wako Ni Dhabihu?
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Desemba 1
    • Watu walitakwa na Sheria watoe matoleo mbalimbali pia kwa ajili yao wenyewe. Matoleo fulani yalikuwa kwa ajili ya dhambi zilizotendwa, mengine kwa ajili ya sababu za kisherehe, na bado mengine kwa sababu ya kujitoa kwao na shukrani zao. Masanduku yaliyotiwa alama ya “Hua-turturi na njiwa wachanga” na “Matoleo ya kuteketeza” yangekuwa ya makusudi hayo. “Ndani ya Tarumbeta ya Tatu,” kinasema kitabu The Temple, Its Ministry and Services, “wale wanawake ambao walipaswa kuleta hua-turturi kwa ajili ya toleo la kuteketeza na toleo la dhambi walitumbukiza pesa zenye kulingana na bei ya hua hao. Na pesa hizo zilichukuliwa kila siku kisha hesabu ya hua-turturi wenye kulingana na pesa hizo wakatolewa kama toleo.” Inaelekea hilo ndilo jambo ambalo wazazi wa kitoto kichanga Yesu walifanya.—Ona Luka 2:22-24; Walawi 12:6-8.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki