-
Jinsi Tunavyoweza Kudumisha Maoni YanayofaaMnara wa Mlinzi—2014 | Machi 15
-
-
8, 9. (a) Mjane mwenye uhitaji alikuwa katika hali gani? (b) Huenda mjane huyo alikuwa na hisia gani zisizofaa?
8 Yesu alimtazama mjane fulani mwenye uhitaji katika hekalu la Yerusalemu. Mfano wa mjane huyo unaweza kutusaidia kudumisha maoni yanayofaa licha ya udhaifu wetu. (Soma Luka 21:1-4.) Fikiria hali za mjane huyo. Alivumilia huzuni ya kufiwa na mume wake na pia alivumilia hali mbaya iliyosababishwa na viongozi wa kidini ‘waliomeza nyumba za wajane’ badala ya kuwasaidia watu hao wanyonge. (Luka 20:47) Alikuwa maskini sana hivi kwamba mchango aliotoa hekaluni ulikuwa sawa na mshahara ambao mfanyakazi angelipwa kwa kufanya kazi kwa dakika chache tu.
9 Hebu wazia jinsi mjane huyo alivyohisi alipoingia kwenye ua wa hekalu akiwa na sarafu zake mbili zenye thamani ndogo. Je, huenda alifikiri kwamba angetoa mchango mkubwa ikiwa mume wake angekuwa hai? Je, aliaibika alipoona wengine waliokuwa mbele yake wakitoa michango mikubwa, pengine akihisi kwamba mchango wake haukuwa na thamani yoyote? Hata ikiwa alihisi hivyo, bado alifanya yote aliyoweza kwa ajili ya ibada ya kweli.
-
-
Jinsi Tunavyoweza Kudumisha Maoni YanayofaaMnara wa Mlinzi—2014 | Machi 15
-
-
11. Unaweza kujifunza nini kutokana na simulizi la mjane?
11 Hali zako zinaweza kuathiri moja kwa moja yale unayoweza kutimiza katika utumishi wa Yehova. Kwa sababu ya umri mkubwa au matatizo ya kiafya, wahubiri fulani hawawezi kuhubiri habari njema kwa saa nyingi. Je, wanapaswa kuhisi kwamba hawastahili kutoa ripoti ya utumishi wao? Hata ikiwa huna matatizo mengi, unaweza kuhisi kwamba jitihada zako hazina thamani zikilinganishwa na jumla ya saa ambazo watu wa Mungu hutumia kila mwaka kumwabudu. Hata hivyo, tunajifunza kutokana na simulizi la mjane maskini kwamba Yehova huona na kuthamini kila jambo tunalofanya katika ibada yake, hasa tunapokabili hali ngumu. Fikiria mambo uliyotimiza katika ibada ya Yehova mwaka uliopita. Je, kuna pindi yoyote ulipohitaji kujidhabihu kwa njia ya pekee ili umtumikie Mungu? Ikiwa ndivyo, uwe na hakika kwamba Yehova anathamini utumishi uliomtolea katika pindi hiyo. Ikiwa unafanya yote unayoweza katika utumishi wa Yehova kama yule mjane mwenye uhitaji, hilo linathibitisha kwamba uko “katika imani.”
-