Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kaisaria na Wakristo wa Mapema
    Mnara wa Mlinzi—1989 | Machi 15
    • Pia ndani ya chumba hicho mna sarafu ndogo mbili za shaba zinazopendeza sana sana. Ya kwanza (upande wa kulia) ina mchoro huu: “Mwaka wa pili wa uhuru wa Sayuni.” Juu ya ile ya pili yapo maneno haya: “Mwaka wa nne hadi kukombolewa kwa Sayuni.” Sarafu hizo zinasemwa na wanachuo kuwa ni za 67 W.K. na 69 W.K. “Uhuru” unaotajwa ulikuwa kipindi ambacho Wayahudi walishikilia Yerusalemu, baada ya Sestio Galo kuondoa majeshi yake ya Kiroma katika mwaka 66 W.K.

      Kuondoka huko kulifanya iwezekane kuikimbia Yerusalemu. Watu walioitikadi Yesu walikimbia, kwa maana alikuwa amesema waziwazi hivi: “Hapo mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo jueni ya kwamba uharibifu wake umekaribia. Ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani, na walio katikati yake wakimbilie nje, na walio katika mashamba wasiuingie.” (Luka 21:20, 21) Inaonekana kwamba wenye kufanyiza sarafu hizo “za ushindi” hawakujua ni uharibifu gani uliowangojea!

  • Kaisaria na Wakristo wa Mapema
    Mnara wa Mlinzi—1989 | Machi 15
    • Kwa hisani ya Jumba la Kuhifadhi Vitu vya Makumbusho ya Historia ya Kiasili la Manispaa ya Los Angeles

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki