-
“Ukombozi Wenu Unakaribia”!Mnara wa Mlinzi—2015 | Julai 15
-
-
2. Wakristo walihitaji kuchukua hatua gani mwaka wa 66 W.K., na hilo liliwezekanaje?
2 Bila shaka unakumbuka maneno ya Yesu yanayopatikana katika Injili ya Luka: “Mtakapoona Yerusalemu limezingirwa na majeshi yaliyopiga kambi, ndipo jueni kwamba kufanywa ukiwa kwake kumekaribia.” (Luka 21:20) Hata hivyo, huenda unajiuliza, ‘Ninawezaje kutii maagizo yanayotolewa katika onyo hilo?’ Yesu alisema hivi pia: “Ndipo wale walio katika Yudea waanze kukimbilia milimani, na wale walio katikati yake na waondoke, nao wale walio katika sehemu za mashambani wasiingie ndani.” (Luka 21:21) Unawezaje kuondoka Yerusalemu wakati jiji limezingirwa? Kisha, jambo la ajabu linatokea. Unaona majeshi ya Roma yanaanza kuondoka! Kama ilivyotabiriwa, shambulizi ‘linafupishwa.’ (Mt. 24:22) Sasa unapata nafasi ya kutii maagizo ya Yesu. Mara moja unakimbia kutoka jijini kuelekea milimani upande mwingine wa Mto Yordani pamoja na Wakristo wengine waaminifu.a Kisha, mwaka wa 70 W.K., jeshi jipya la Roma linaingia Yerusalemu na kuliharibu jiji. Lakini unasalimika kwa sababu ulitii maagizo ya Yesu.
-
-
“Ukombozi Wenu Unakaribia”!Mnara wa Mlinzi—2015 | Julai 15
-
-
WAKATI WA MAJARIBU NA HUKUMU
7, 8. Tutakuwa na nafasi ya kufanya nini baada ya kuharibiwa kwa dini za uwongo? Na ni kwa njia gani watu wa Mungu watakuwa tofauti na watu wengine?
7 Ni nini kitakachotokea baada ya uharibifu wa dini za uwongo? Huo utakuwa wakati wa kufunua kile kilicho moyoni mwetu. Watu wengi watatafuta kimbilio katika mashirika ya kibinadamu yanayofananishwa na “miamba ya milima.” (Ufu. 6:15-17) Hata hivyo, watu wa Mungu watamkimbilia Yehova ili kupata ulinzi. Katika karne ya kwanza, kufupishwa kwa dhiki hakukuwa wakati wa Wayahudi wengi kugeuzwa kuwa Wakristo. Huo ulikuwa wakati wa wale ambao tayari walikuwa Wakristo kutii na kutenda. Vivyo hivyo, hatutarajii kwamba dhiki kuu itakapofupishwa wakati ujao watu wengi watabadilika ghafla na kuwa Wakristo wa kweli. Badala yake, hiyo itakuwa fursa ya waabudu wa kweli kuthibitisha upendo wao kwa Yehova na kuwaunga mkono ndugu za Kristo.—Mt. 25:34-40.
8 Hatujui kikamili mambo yote yatakayotokea wakati huo wa majaribu. Hata hivyo, tunajua kwamba tutahitaji kujidhabihu. Wakristo katika karne ya kwanza walihitaji kuacha mali zao na kuvumilia hali ngumu ili waokoke. (Marko 13:15-18) Je, tutakuwa tayari kupoteza vitu vya kimwili ili tuendelee kuwa waaminifu? Je, tutakuwa tayari kufanya chochote kinachohitajika ili tuendelee kuwa washikamanifu kwa Yehova? Hebu wazia! Wakati huo, ni sisi pekee tutakaofuata mfano wa nabii Danieli wa kale kwa kuendelea kumwabudu Mungu chini ya hali zozote zile.—Dan. 6:10, 11.
-