Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Ni Nini Itakayokuwa Ishara ya Kuwapo Kwako?”
    Mnara wa Mlinzi—1994 | Februari 15
    • 16. Luka 21:24 laongeza jambo jipi kwenye unabii wa Yesu, na hilo lina umaana gani?

      16 Tukilinganisha Mathayo 24:15-28 na Marko 13:14-23 pamoja na Luka 21:20-24, twapata kionyeshi cha pili kwamba utabiri wa Yesu ulihusisha muda mrefu baada ya uharibifu wa Yerusalemu. Kumbuka kwamba Luka pekee ndiye aliyekuwa ametaja tauni. Vivyo hivyo, ni yeye pekee aliyemalizia sehemu hiyo kwa maneno haya ya Yesu: “Yerusalemu litakanyagwa-kanyagwa na mataifa, hata nyakati zilizowekwa za mataifa [“nyakati za Wasio Wayahudi,” King James Version] ziwe zimetimizwa.”e (Luka 21:24, NW) Wababiloni walimwondoa mfalme wa mwisho wa Wayahudi katika 607 K.W.K., na baada ya hapo, Yerusalemu, likifananisha Ufalme wa Mungu, lilikanyangwa-kanyagwa. (2 Wafalme 25:1-26; 1 Mambo ya Nyakati 29:23; Ezekieli 21:25-27) Kwenye Luka 21:24, Yesu alionyesha kwamba hali hiyo ingeendelea hadi wakati ujao mpaka wakati ungefika ambapo Mungu angesimamisha Ufalme tena.

  • “Ni Nini Itakayokuwa Ishara ya Kuwapo Kwako?”
    Mnara wa Mlinzi—1994 | Februari 15
    • e Wengi huona katika simulizi la Luka badiliko la mkazo baada ya Luka 21:24. Dakt. Leon Morris asema: “Yesu aendelea kusema juu ya nyakati za Wasio Wayahudi. . . . Kulingana na maoni ya wasomi walio wengi fikira yaelekezwa sasa kwenye kuja kwa Mwana wa Adamu.” Profesa R. Ginns aandika hivi: “Kuja kwa Mwana wa Adamu—(Mt 24:29-31; Mk 13:24-27). Kutajwa kwa ‘nyakati za Wasio Wayahudi’ kwaandaa utangulizi kwa kichwa hicho; sasa maoni ya [Luka] yanafikia muda mrefu baada ya kuharibiwa kwa Yerusalemu kuingia katika wakati ujao.”

      f Profesa Walter L. Liefeld aandika hivi: “Kwa hakika yawezekana kuona kwamba tabiri za Yesu zilitia ndani sehemu mbili: (1) matukio ya A.D. 70 yaliyohusisha hekalu na (2) yale ya muda mrefu baadaye katika wakati ujao, yanayoelezwa katika maneno ya kiapokalipsi [ufunuo] zaidi.” Ufafanuzi uliohaririwa na J. R. Dummelow wasema hivi: “Mengi ya magumu mazito zaidi ya hotuba hiyo kuu hutoweka inapong’amuliwa kwamba Bwana yetu hakurejezea ndani yayo tukio moja bali mawili, na kwamba lile la kwanza lilifananisha lile la pili. . . . [Luka] 21:24 hasa, linalosema juu ya ‘nyakati za Wasio Wayahudi,’ . . . laweka kipindi cha katikati kisicho dhahiri kati ya anguko la Yerusalemu na mwisho wa ulimwengu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki