Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kusaidia Mtoto Akue Katika Hekima ya Kutii Mungu
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Februari 15
    • “Sasa wazazi wake walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu mwaka baada ya mwaka kwa ajili ya sikukuu ya kupitwa.” (Luka 2:41, NW) Kulingana na Sheria ya Mungu, kila mwanamume alipaswa aonekane Yerusalemu kwa ajili ya sikukuu zilizokuwa zikifanywa. (Kumbukumbu 16:16) Lakini maandishi yanasema kwamba “wazazi wake walikuwa na desturi ya kwenda.” Yusufu alienda na Mariamu, na inaelekea pamoja na wale wengine katika jamaa hiyo, katika safari hiyo ya kilometa 100 kwenda Yerusalemu kwa ajili ya pindi hiyo yenye furaha. (Kumbukumbu 16:6, 11) Ilikuwa desturi yao—sehemu ya kawaida ya maisha zao. Pia, wao hawakujitokeza kule mradi tu waonekane wamefika; wao walibaki kwa ajili ya siku zote za sikukuu hiyo.—Luka 2:42, 43.

  • Kusaidia Mtoto Akue Katika Hekima ya Kutii Mungu
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Februari 15
    • Kosa la Kupitiwa Tu

      Wakati Yesu alipokuwa mwenye umri mdogo zaidi, bila shaka alikaa karibu na wazazi wake wakati wa safari hizo za kila mwaka za kwenda kwenye ule mji mkubwa wa Yerusalemu. Ijapokuwa hivyo, alipoendelea kuwa na umri mkubwa zaidi huenda akawa alipewa uhuru zaidi kidogo. Alipokuwa na umri wa miaka 12, alikuwa karibu na umri ambao Wayahudi wanauona kuwa hatua ya maana katika kijia cha kuelekea uanaume. Labda kwa sababu ya badiliko hilo lililo la kikawaida na kiasili, kosa la kupitiwa tu lilitukia wakati ulipofika jamaa ya Yusufu iondoke Yerusalemu na kurudi nyumbani. Usimulizi unasema: “Lakini walipokuwa wakirudi, mvulana Yesu alibaki nyuma katika Yerusalemu, na wazazi wake hawakutambua jambo hilo. Kwa kudhani kwamba yeye alikuwa katika shirika hilo wakiwa wanasafiri pamoja, walimaliza umbali wa siku moja, ndipo wakaanza kumtafuta sana miongoni mwa watu wa ukoo na wazoeani wao.”​—Luka 2:43, 44, NW.

      Kuna mambo fulani ya kituko hicho ambayo wazazi na hata watoto watatambua. Ijapokuwa hivyo, kuna tofauti moja: Yesu alikuwa mkamilifu. Kwa kuwa yeye alikuwa akijitiisha kwa kuwasikia Yusufu na Mariamu, hatuwezi kuwazia kwamba yeye alishindwa kutii mpango fulani waliokuwa wamefanya pamoja naye. (Luka 2:52) Inaelekea zaidi sana kwamba kulikuwa na mvunjiko fulani wa kupashana habari. Wazazi walidhani kwamba Yesu alikuwa katika shirika lile la watu wa ukoo na wazoeani wao. (Luka 2:44) Ni jambo rahisi kuwazia kwamba katika pirika-pirika za kuondoka Yerusalemu, wao wangeelekeza fikira kwanza kwenye watoto wao wachanga zaidi na kudhani kwamba mwana wao mwenye umri mkubwa zaidi, Yesu, alikuwa pia akiambatana nao.

      Ijapokuwa hivyo, kwa wazi Yesu alifikiri kwamba wazazi wake wangejua alikokuwa. Jambo hilo linadokezwa na jibu lake la baadaye: “Mbona ninyi mlilazimika kwenda mkinitafuta mimi? Je! ninyi hamkujua kwamba ni lazima niwe katika nyumba ya Baba yangu?” Yeye hakuwa akikosa kuonyesha heshima. Maneno yake yanafunua tu mshangao wake juu ya uhakika wa kwamba wazazi wake hawakujua walikopaswa kumtafuta. Hicho kilikuwa kisa chenye kuonyesha kawaida ya kutofahamiana ambako wazazi wengi wenye watoto wanaokua wanaweza kuthamini.​—Luka 2:49, NW.

      Fikiria hangaiko la Yusufu na Mariamu usiku ule wa kwanza, wakati wao walipopata kujua kwamba Yesu hayupo. Na wazia wasiwasi wao wenye kuongezeka wakati wa zile siku mbili walizomtafuta Yerusalemu. Ijapokuwa hivyo, mambo yakawa kwamba mazoezi waliyokuwa wamempa yaliwapa malipo katika jambo hili lenye hatari. Yesu hakuwa ameingia katika shirika fulani baya. Yeye hakuwa akiletea wazazi wake aibu. Wao walipomkuta Yesu, alikuwa “katika hekalu, akiwa ameketi katikati ya walimu na kuwasikiliza na kuwauliza maswali. Lakini wote wale waliokuwa wanamsikiliza walikuwa wakiendelea kustaajabia ufahamu wake na majibu yake.”—Luka 2:46, 47, NW.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki