-
Yesu Anasali Akiwa na Huzuni NyingiYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Yesu anahangaishwa sana na jinsi kifo chake kama mhalifu kitakavyoliletea suto jina la Baba yake. Ingawa hivyo, Yehova anasikiliza sala ya Mwana wake, na pindi moja Mungu anamtuma malaika ili amtie nguvu. Hata hivyo, Yesu haachi kumsihi Baba yake, bali anaendelea “kusali kwa bidii zaidi.” Ana mkazo mwingi sana wa kihisia. Yesu amebeba jukumu zito sana! Uhai wake mwenyewe wa milele na uhai wa wanadamu wenye imani unahusika. Hata ‘jasho lake linakuwa kama matone ya damu yakidondoka chini.’—Luka 22:44.
-