-
Mkazo Unaweza Kudhibitiwa!Amkeni!—1998 | Machi 22
-
-
Usikate kauli kwamba umekataliwa na Mungu. Biblia yatuambia kwamba kwa miaka mingi, Hana, aliyekuwa mwanamke mwaminifu, alikuwa na ‘uchungu rohoni mwake’ (“alihuzunika sana,” Revised Standard Version). (1 Samweli 1:4-11) Katika Makedonia, Paulo “alikuwa na mkazo katika kila hali.” (2 Wakorintho 7:5, Byington) Kabla ya kifo chake, Yesu “alikuwa akiingia katika maumivu makali,” na mkazo wake ulikuwa mkubwa sana hivi kwamba “jasho lake likawa kama matone ya damu yakianguka kwenye ardhi.”a (Luka 22:44) Hao walikuwa watumishi waaminifu wa Mungu. Kwa hiyo, unapokabili mkazo hakuna sababu ya kukata kauli kwamba Mungu amekuacha.
-
-
Mkazo Unaweza Kudhibitiwa!Amkeni!—1998 | Machi 22
-
-
a Jasho lenye damu limeripotiwa kuwa limetukia katika visa fulani vya mkazo wa akili ulio mkali sana. Kwa kielelezo, katika hali ya hematidrosis, kuna kutoka kwa jasho lililochangamana na damu au rangi ya damu au umajimaji wa mwili uliochangamana na damu. Hata hivyo, haiwezi kusemwa kwa uhakika kabisa, jambo hususa ambalo lilitukia katika kisa cha Yesu.
-