Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kitabu Cha Biblia 42—Luka
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 1. Luka aliandika Gospeli ya aina gani?

      GOSPELI ya Luka iliandikwa na mwanamume aliyekuwa na akili yenye makini na moyo wenye fadhili, na mchanganyiko huo mzuri wa sifa, pamoja na uongozi wa roho ya Mungu, umetokeza simulizi lililo sahihi na lenye kujaa uchangamfu na hisia. Katika mistari ya ufunguzi, yeye asema, “nimeona vema mimi nami, kwa kuwa nimejitafutia usahihi wa mambo hayo yote tangu mwanzo, kukuandikia kwa taratibu.” Utoaji wake wenye habari nyingi, wenye uangalifu wathibitisha dai hilo kikamili.—Luka 1:3.

  • Kitabu Cha Biblia 42—Luka
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 4. Yawezekana, Luka iliandikwa lini, na ni hali gani zinazounga mkono maoni hayo?

      4 Luka aliandika Gospeli yake lini? Matendo 1:1 hudokeza kwamba mwandikaji wa Matendo (ambaye alikuwa Luka pia) hapo mapema zaidi alikuwa ametunga “kitabu kile cha kwanza,” ile Gospeli. Yawezekana sana Matendo kilikamilishwa karibu 61 W.K. Luka akiwa katika Rumi pamoja na Paulo, aliyekuwa akingojea rufani yake kwa Kaisari. Kwa hiyo simulizi la Gospeli hiyo lawezekana liliandikwa na Luka katika Kaisaria karibu 56-58 W.K., baada ya yeye kurejea na Paulo kutoka Filipi mwishoni mwa safari ya umisionari ya tatu ya Paulo na wakati ambao Paulo alikuwa akingojea miaka miwili gerezani kule Kaisaria kabla ya kupelekwa Rumi kwa ajili ya rufani yake. Kwa kuwa Luka alikuwa huko katika Palestina, wakati huu yeye alikuwa katika hali nzuri ya ‘kutafuta kwa usahihi mambo tangu mwanzo’ kuhusu uhai na huduma ya Yesu. Kwa hiyo, simulizi la Luka laonekana lilitangulia Gospeli ya Marko.

      5. Yawezekana Luka ‘alifuatia kwa usahihi’ matukio ya uhai wa Yesu kupitia vyanzo gani?

      5 Bila shaka, Luka hakuwa shahidi aliyejionea matukio yote anayoandika katika Gospeli yake, akiwa hakuwa mmoja wa wale 12 na yawezekana hata hakuwa mwamini mpaka baada ya kifo cha Yesu. Hata hivyo, yeye alishirikiana karibu sana na Paulo katika shamba la umisionari. (2 Tim. 4:11; Flm. 24) Kwa hiyo, kama ambavyo yaweza kutazamiwa, uandikaji wake waonyesha uthibitisho wa uvutano wa Paulo, kama inavyoweza kuonekana kwa kulinganisha masimulizi mawili yao ya Chakula cha Jioni cha Bwana, katika Luka 22:19, 20 na 1 Wakorintho 11:23-25. Kikiwa chanzo zaidi cha habari, Luka angeweza kurejezea Gospeli ya Mathayo. Katika ‘kutafuta kwa usahihi mambo,’ yeye angeweza kibinafsi kuuliza mashahidi wengi waliojionea matukio ya maisha ya Yesu, kama vile wanafunzi waliokuwapo na yawezekana mama ya Yesu, Mariamu. Twaweza kuwa na uhakika kwamba yeye alifanya kila liwezekanalo katika kukusanya habari za kirefu zenye kutegemeka.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki