Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yesu Ni Nani?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 4. Yesu si Mungu Mweza Yote

      Ingawa Yesu ni kiumbe wa roho mwenye nguvu mbinguni, Biblia inafundisha kwamba anajitiisha kwa Yehova ambaye ni Mungu wake na Baba yake. Kwa nini tunasema hivyo? Onyesha VIDEO ili uone kile ambacho Biblia inafundisha kuhusu tofauti kati ya cheo cha Yesu na Mungu mweza yote.

      VIDEO: Je, Yesu Kristo Ni Mungu? (3:22)

      Maandiko yanayofuata yanatusaidia kuelewa uhusiano uliopo kati ya Yehova na Yesu. Soma kila andiko kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

      Soma Luka 1:30-32.

      • Malaika alifafanuaje uhusiano uliopo kati ya Yesu na Yehova Mungu, “Aliye Juu Zaidi”?

      Soma Mathayo 3:16, 17.

      • Yesu alipobatizwa, sauti kutoka mbinguni ilisema nini?

      • Unafikiri ilikuwa sauti ya nani?

      Soma Yohana 14:28.

      • Ni nani aliye na umri mkubwa na mwenye mamlaka zaidi? Je, ni baba au mwana?

      • Yesu alisema Yehova ni Baba yake, hilo linatufundisha nini?

      Soma Yohana 12:49.

      • Je, Yesu anahisi kwamba yeye na Baba yake ni mtu yuleyule? Wewe una maoni gani?

  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • Somo la 31. Yesu Kristo Mfalme aliye mbinguni akiwa mbele ya utukufu wa Yehova.

      SOMO LA 31

      Ufalme wa Mungu Ni Nini?

      Ufalme wa Mungu ndio ujumbe muhimu zaidi katika Biblia. Yehova atatumia Ufalme huo kutimiza kusudi lake la mwanzoni la kuifanya dunia iwe paradiso. Ufalme huo ni nini? Tunajuaje kwamba umeanza kutawala? Ufalme huo umetimiza mambo gani? Na utatimiza mambo gani wakati ujao? Maswali hayo yatajibiwa katika somo hili na masomo mawili yanayofuata.

      1. Ufalme wa Mungu ni nini, na Mfalme wake ni nani?

      Ufalme huo ni serikali iliyoanzishwa na Yehova Mungu mwenyewe. Mfalme wa Ufalme huo ni Yesu Kristo, na anatawala kutoka mbinguni. (Mathayo 4:17; Yohana 18:36) Biblia inasema hivi kumhusu Yesu: “Atatawala akiwa Mfalme . . . milele.” (Luka 1:32, 33) Akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu, Yesu atatawala watu wote duniani.

      2. Ni nani wanaotawala pamoja na Yesu?

      Yesu anatawala pamoja na wengine. “Watu kutoka katika kila kabila na lugha na watu na taifa . . . watatawala wakiwa wafalme juu ya dunia.” (Ufunuo 5:9, 10) Ni watu wangapi watakaotawala pamoja na Kristo? Tangu Yesu alipokuja duniani, mamilioni ya watu wamekuwa wafuasi wake. Lakini watu 144,000 ndio tu wanaoenda mbinguni kutawala pamoja na Yesu. (Soma Ufunuo 14:1-4.) Wakristo wengine wote walio duniani watakuwa raia wa Ufalme huo.​—Zaburi 37:29.

      3. Kwa nini Ufalme wa Mungu ni bora kuliko serikali za wanadamu?

      Ingawa watawala wa serikali za wanadamu wanajitahidi kufanya mambo mazuri, hawana uwezo wa kufanya mambo yote wanayotaka. Baada ya kipindi chao cha kutawala kwisha, huenda watawala wengine wabinafsi wakaanza kutawala na hawawajali raia wao. Lakini kuhusu Yesu Mtawala wa Ufalme wa Mungu, hakuna mtawala mwingine atakayechukua nafasi yake. Mungu “[ameusimamisha] ufalme ambao hautaangamizwa kamwe.” (Danieli 2:44) Yesu atatawala dunia yote, na hatakuwa na ubaguzi. Yesu ni mwenye upendo, fadhili, na haki, naye atawafundisha watu kuwatendea wengine kwa njia hiyohiyo, yaani, kwa upendo, fadhili, na haki.​—Soma Isaya 11:9.

      CHIMBA ZAIDI

      Chunguza uone kwa nini Ufalme wa Mungu ni serikali bora kuliko serikali zote za wanadamu.

      Yesu Kristo akiitawala dunia akiwa kwenye kiti chake cha ufalme mbinguni. Watawala wenzake wameketi nyuma yake. Nuru ya Yehova inaangaza nyuma yao.

      4. Serikali yenye nguvu itaitawala dunia yote

      Yesu Kristo ana nguvu nyingi sana za kutawala kuliko mtawala yeyote katika historia. Soma Mathayo 28:18, kisha mzungumzie swali hili:

      • Kwa nini Yesu ana mamlaka kubwa zaidi kuliko mtawala yeyote wa serikali za wanadamu?

      Serikali za wanadamu hubadilika-badilika, na kila serikali hutawala sehemu fulani ya dunia. Namna gani Ufalme wa Mungu? Soma Danieli 7:14, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Kwa nini inafurahisha kujua kwamba Ufalme wa Mungu “hautaangamizwa”?

      • Kwa nini tunafurahi kujua kwamba utaitawala dunia yote?

      5. Ni lazima serikali za wanadamu ziondolewe

      Kwa nini ni lazima Ufalme wa Mungu uondoe serikali za wanadamu? Onyesha video, kisha mzungumzie swali linalofuata.

      VIDEO: Ufalme wa Mungu Ni Nini?​—Kisehemu (1:41)

      • Utawala wa serikali za wanadamu umekuwa na matokeo gani?

      Soma Mhubiri 8:9, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Je, unafikiri Ufalme wa Mungu unapaswa kuondoa serikali za wanadamu? Kwa nini?

      6. Watawala wa Ufalme wa Mungu wanaelewa hali yetu

      Kwa kuwa Mfalme wetu, Yesu, aliwahi kuwa mwanadamu, anaweza ‘kuusikitikia udhaifu wetu.’ (Waebrania 4:15) Wanaume na wanawake waaminifu 144,000 ambao watatawala pamoja na Yesu wamechaguliwa na Yehova “kutoka katika kila kabila na lugha na watu na taifa.”​—Ufunuo 5:9.

      • Je, unafarijika kujua kwamba Yesu na watawala wenzake wanaelewa hali za wanadamu? Kwa nini?

      Wanaume na wanawake watiwa mafuta kutoka malezi mbalimbali ambao waliishi katika vipindi tofauti.

      Yehova amewachagua wanaume na wanawake kutoka katika malezi mbalimbali watawale pamoja na Yesu

      7. Sheria za Ufalme wa Mungu ni bora zaidi

      Serikali huweka sheria ambazo zimekusudiwa kuwanufaisha na kuwalinda raia wake. Ufalme wa Mungu pia una sheria ambazo zinapaswa kufuatwa na raia wake. Soma 1 Wakorintho 6:9-11, kisha mzungumzie maswali haya:

      • Unafikiri ulimwengu utakuwaje kila mtu atakapofuata sheria za Mungu?a

      • Je, unafikiri Yehova ana haki ya kuwawekea sheria raia wa Ufalme wake? Kwa nini?

      • Ni nini kinachoonyesha kwamba watu ambao hawafuati sheria hizo wanaweza kubadilika?​—Ona mstari wa 11.

      Polisi akielekeza magari barabarani. Watu wenye umri mbalimbali wakivuka barabara.

      Serikali huweka sheria ili kuwalinda na kuwanufaisha raia wake. Ufalme wa Mungu una sheria bora zinazowalinda na kuwanufaisha raia wake

      HUENDA MTU AKAULIZA: “Ufalme wa Mungu ni nini?”

      • Unawezaje kujibu swali hilo?

      MUHTASARI

      Ufalme wa Mungu ni serikali halisi iliyo mbinguni ambayo itaitawala dunia yote.

      Ungejibuje?

      • Watawala wa Ufalme wa Mungu ni nani?

      • Kwa nini Ufalme wa Mungu ni bora kuliko serikali zote za wanadamu?

      • Yehova anatarajia raia wa Ufalme wake wafanye mambo gani?

      Lengo

      CHUNGUZA ZAIDI

      Chunguza uone Yesu alisema utawala wa Mungu utatawala kutokea wapi.

      “Je, Ufalme wa Mungu Umo Moyoni Mwako?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

      Kwa nini Mashahidi wa Yehova wanachagua kuwa washikamanifu kwa Ufalme wa Mungu badala ya serikali za wanadamu?

      Kuunga Mkono Ufalme wa Mungu (1:43)

      Chunguza jinsi Biblia inavyofafanua wale 144,000 ambao wamechaguliwa na Yehova kutawala pamoja na Yesu.

      “Ni Nani Wanaoenda Mbinguni?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

      Ni nini kilichomsadikishia mwanamke aliyekuwa gerezani kwamba Mungu peke yake ndiye anayeweza kuleta ulimwengu wenye haki?

      “Jinsi Nilivyopata Suluhisho la Ukosefu wa Haki” (Amkeni!, Novemba 2011)

      a Baadhi ya sheria hizo zitazungumziwa katika Sehemu ya 3.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki