Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yesu Kristo
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
    • Maandishi yaliyoongozwa na roho yanasema hivi: “Lakini kuzaliwa kwa Yesu Kristo kulikuwa katika njia hii. Katika wakati ambapo Maria mama yake alikuwa amechumbiwa na Yosefu, alionekana kuwa ana mimba kwa njia ya roho takatifu kabla ya wao kuungana pamoja.” (Mt 1:18) Kabla ya hilo, mjumbe wa kimalaika wa Yehova alikuwa amemwambia msichana bikira Maria kwamba ‘angechukua mimba katika tumbo lake la uzazi’ kama tokeo la roho takatifu ya Mungu kuja juu yake na nguvu Zake kumfunika. (Lu 1:30, 31, 34, 35) Kwa kuwa mimba halisi ilitokea, inaonekana kwamba Yehova Mungu alifanya seli ya mbegu ya kike, ndani ya tumbo la uzazi la Maria irutubishwe, akatimiza hilo kwa kuuhamisha uhai wa Mwana wake mzaliwa wa kwanza kutoka makao ya roho hadi duniani. (Gal 4:4) Ni katika njia hiyo tu kwamba yule mtoto ambaye angezaliwa angeweza kudumisha kitambulisho cha kuwa mtu yule yule mmoja aliyekuwa amekaa mbinguni akiwa yule Neno, na ni katika njia hiyo tu kwamba hatimaye angeweza kuwa mwana halisi wa Maria na kwa hivyo mzao wa kweli wa mababu za Maria, yaani, Abrahamu, Isaka, Yakobo, Yuda, na Mfalme Daudi na awe mrithi halali wa ahadi za kimungu walizopewa. (Mwa 22:15-18; 26:24; 28:10-14; 49:10; 2Sa 7:8, 11-16; Lu 3:23-34; ona GENEALOGY OF JESUS CHRIST.) Kwa hiyo, inawezekana kwamba mtoto huyo aliyezaliwa alifanana na mama yake Myahudi katika sifa fulani za kimwili.

      Maria alikuwa mzao wa Adamu mtenda-dhambi, kwa hiyo yeye mwenyewe alikuwa asiyekamilika na mwenye dhambi. Basi swali linatokezwa, ni jinsi gani Yesu, “mzaliwa wa kwanza” wa Maria (Lu 2:7), angeweza kuwa mkamilifu na bila dhambi akiwa kiumbehai chenye mwili. Japo wataalamu wa chembe za urithi wamejifunza mengi juu ya sheria za urithi na kuhusu tabia za urithi zenye kutawala kimaumbile na zile zinazotawaliwa kimaumbile, hawajawa na uzoefu wowote wa kujifunza juu ya matokeo ya kuunganisha ukamilifu na kutokamilika, kama ilivyokuwa katika utungaji wa mimba ya Yesu. Kulingana na matokeo yanayofunuliwa katika Biblia, inaonekana kwamba kani-uhai kamilifu (iliyotokeza utungaji-mimba) ilifunika kabisa kutokamilika kokote ambako kulikuwa ndani ya seli ya mbegu ya kike ya Maria, na hivyo kutokeza kiolezo cha kiurithi (na ukuzi wa kiini-tete) kilichokuwa kikamilifu tangu mwanzoni. Vyovyote vile, utendaji wa roho takatifu ya Mungu pindi hiyo, ulihakikisha kufanikiwa kwa kusudi la Mungu. Ni kama ambavyo malaika Gabrieli alivyomweleza Maria, “nguvu za Aliye Juu Zaidi” zilimfunika hivi kwamba kilichozaliwa kilikuwa kitakatifu, Mwana wa Mungu. Ni kana kwamba roho takatifu ya Mungu ilifanyiza ukuta wenye kutoa himaya ili kuzuia hali yoyote ya kutokamilika au uvutano ambao ungeweza kuleta madhara, au kutia waa, kiini-tete kilichokuwa kinakua, kuanzia na utungaji-mimba na kuendelea.—Lu 1:35.

  • Roho
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
    • Ni tofauti na “uwezo.” Kwa hiyo, ru′ach na pneu′ma yanapotumiwa kuhusiana na roho takatifu ya Mungu, hurejezea kani (nguvu) ya utendaji isiyoonekana ya Mungu ambayo kupitia hiyo yeye hutimiza kusudi na mapenzi yake ya kimungu. Ni “takatifu” kwa sababu inatoka Kwake, chanzo chake si cha kidunia, nayo ikiwa ni “roho ya utakatifu” haina ufisadi wowote. (Ro 1:4) Hiyo si “uwezo” wa Yehova, kwa maana neno hili la Kiswahili linatafsiri kwa usahihi zaidi maneno mengine katika lugha za awali (Kieb., ko′ach; Kigr., dy′na·mis). Ru′ach na pneu′ma yanatumiwa kwa kukaribiana sana au hata kwa njia iliyo sambamba na maneno hayo yanayomaanisha “uwezo,” jambo ambalo linaonyesha kuwa kuna ukamatano kati ya hayo na bado yana tofauti iliyo dhahiri. (Mik 3:8; Zek 4:6; Lu 1:17, 35; Mdo 10:38) Kimsingi “uwezo” ni kuwa na uweza wa kutenda au kufanya mambo na unaweza kuwa usiotumika, bwete, au usiotenda ukiwa ndani ya mtu fulani au kitu fulani. Kwa upande mwingine, kihususa kani (“nguvu”) linaeleza nishati inayoelekezwa na kutumikishwa juu ya watu au vitu, na laweza kufafanuliwa kuwa “uvutano unaotokeza au unaoelekea kutokeza mtukuto, au badiliko katika mtukuto.” “Uwezo” waweza kufananishwa na nishati iliyowekwa akiba ndani ya betri, na hali kani lingeweza kulinganishwa na mkondo wa umeme unaotoka kwenye betri hiyo. Kwa hiyo, kani (“nguvu”) linawakilisha kwa usahihi zaidi maana ya maneno ya Kiebrania na Kigiriki yanayohusu roho ya Mungu, na hilo linathibitishwa kwa kuyachunguza Maandiko.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki