-
Ni Akina Nani Walio na Furaha Kweli Kweli?Mnara wa Mlinzi—1986 | Oktoba 1
-
-
Akielekeza maelezo yake kwa wanafunzi wake, Yesu anaanza hivi: “Wenye furaha ni ninyi maskini, kwa sababu ufalme wa Mungu ni wenu. Wenye furaha ni ninyi mnaoona njaa sasa, kwa sababu mtajazwa. Wenye furaha ni ninyi mnaolia sasa, kwa sababu mtacheka. ‘Wenye furaha ni ninyi wakati wo wote watu wanapowachukia . . . Furahini siku hiyo na kuruka, kwa maana, tazameni! thawabu yenu ni kuu mbinguni.”
-
-
Ni Akina Nani Walio na Furaha Kweli Kweli?Mnara wa Mlinzi—1986 | Oktoba 1
-
-
Lakini, analomaanisha Yesu juu ya kuwa wenye furaha si kufanya shangwe wala kucheka-cheka, kama wakati mtu anapokuwa na mambo ya kumfurahisha-furahisha. Furaha ya kweli ina kina kirefu zaidi, ina wazo la kuridhika, mtu kujisikia ametosheka na anatimiza mambo maishani.
-
-
Ni Akina Nani Walio na Furaha Kweli Kweli?Mnara wa Mlinzi—1986 | Oktoba 1
-
-
Yesu anamaanisha nini? Kwa sababu gani kuwa na mali, kufuatia anasa kwa kucheka, na kufurahia sifa za wanadamu kunaleta ole? Ni kwa sababu wakati mtu anapokuwa na vitu hivyo na kuvithamini sana, utumishi kwa Mungu, ambao ndio pekee unaoleta furaha ya kweli, unaondolewa katika maisha yake. Wakati ule ule, Yesu hakumaanisha kwamba kuwa maskini tu, mwenye njaa, na mwenye kuomboleza ndiko kunafanya mtu awe mwenye furaha. Lakini, mara nyingi watu hawa wenye hali za shida wanaweza kuitikia mafundisho ya Yesu, na kwa njia hiyo wao wanabarikiwa kupata furaha ya kweli.
-