-
Kunyamazisha Dhoruba InayotishaMnara wa Mlinzi—1987 | Mei 1
-
-
Inaeleweka kwamba Yesu amechoka. Kwa hiyo, upesi baada ya wao kung’oka, yeye analala katika sehemu ya nyuma ya mashua, analaza kichwa chake juu ya mto, na kulala fofofo. Baadhi ya mitume ni mabaharia wenye ujuzi, kwa maana wamekwisha kuvua sana samaki katika Bahari ya Galilaya. Kwa hiyo wao wanalitwaa daraka la kuisafirisha mashua baharini.
Lakini hii haitakuwa safari rahisi. Kwa sababu joto ni jingi zaidi kwenye uso wa ziwa ulio karibu kilometa 210 (futi 700) chini ya usawa wa bahari, na kwa sababu hewa ni baridi zaidi katika milima ya karibu-karibu, nyakati nyingine pepo zenye nguvu zinavuma kuteremka chini na kufanyiza dhoruba kali-kali za ghafula juu ya ziwa. Hilo ndilo jambo linalotukia sasa. Upesi mawingu yanaanza kukumba-kumba mashua na kurusha maji ndani, hivi kwamba inakaribia kujawa kabisa na maji. Hata hivyo, Yesu anaendelea kulala!
-
-
Kunyamazisha Dhoruba InayotishaMnara wa Mlinzi—1987 | Mei 1
-
-
[Picha ya ukurasa mzima katika ukurasa wa 8]
-