-
Je! Wewe ni Mwenye Matokeo Katika Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko?Mnara wa Mlinzi—1986 | Machi 1
-
-
8. (a) “Mtu fulani mwenye ustadi katika Sheria” alimuuliza Yesu ulizo gani? (b) Yesu alishughulikaje na ulizo hilo, na kwa sababu gani?
8 Katika Luka sura ya 10, mistari 25-28 (NW) tunasoma juu ya “mtu fulani mwenye ustadi katika Sheria” aliyetaka kumjaribu Yesu kwa kuuliza: “Mwalimu, ni kwa kufanya nini nitarithi uzima wa milele?” Wewe ungalijibuje? Yesu alifanya nini? Angaliweza kwa urahisi kutoa jibu la moja kwa moja, lakini alitambua kwamba mtu huyo tayari alikuwa na maoni fulani juu ya jambo hilo. Kwa hiyo Yesu akamuuliza ni jinsi gani yeye angejibu ulizo hilo, akisema: “Imeandikwa nini katika ile Sheria? Wewe unasomaje?” Mtu huyo akajibu: “‘Ni lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili zako zote,’ na, ‘jirani yako kama wewe mwenyewe.’” Yesu akaitikia: “Umejibu kwa usahihi,” halafu, akitaja Mambo ya Walawi 18:5 kwa ufupi, akasema: “Endelea kufanya hivyo na utapata uzima.” Katika pindi nyingine Yesu mwenyewe aliyataja maneno ya amri hizo mbili kwa kujibu ulizo fulani. (Marko 12:28-31, NW) Lakini safari hii mtu aliyekuwa akisema naye aliijua Sheria ya Musa na kwa wazi alitaka kuona kama Yesu alikubaliana na mambo ambayo yeye alikuwa amejifunza kutokana na Sheria hiyo. Yesu alimwacha mtu huyo apate uradhi wa kutoa jibu yeye mwenyewe.
-
-
Je! Wewe ni Mwenye Matokeo Katika Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko?Mnara wa Mlinzi—1986 | Machi 1
-
-
10. (a) Tunaweza kujifunza nini kutokana na mfano huo wa kufundisha? (b) Tunaweza kutumiaje baadhi ya mambo hayo tunapofuata Kichwa cha Mazungumzo yetu ya sasa katika huduma ya shambani?
10 Tunaweza kujifunza nini kutokana na kiolezo hicho cha kufundisha? Je, umeyaona mambo yanayofuata? (1) Yesu alielekeza fikira kwenye Maandiko alipokuwa akitoa jibu kwa ulizo la kwanza la mtu yule. (2) Mtu huyo alikaribishwa na Yesu atoe maoni yake, naye alisifiwa kwa uchangamfu alipotoa elezo lenye ufahamu. (3) Yesu alihakikisha kuendelea kukaza fikira za mtu huyo uhusiano kati ya ulizo na maandiko, kama inavyoonyeshwa katika mstari wa 28. (4) Mfano wenye kuvuta moyo ulitumiwa kuhakikisha kwamba mtu huyo hakuikosa maana hasa ya jibu lililotolewa. Kufuata kiolezo hicho kunaweza kutusaidia tuwatolee wengine sababu za Maandiko kwa matokeo mazuri.
-