-
Mtumikie Yehova Bila KukengeukaMnara wa Mlinzi—2015 | Oktoba 15
-
-
‘Maria aliendelea kulisikiliza neno lake Yesu. Martha alikengeushwa na kazi nyingi.’ —LUKA 10:39, 40.
-
-
Mtumikie Yehova Bila KukengeukaMnara wa Mlinzi—2015 | Oktoba 15
-
-
2 Yesu alimpenda Martha kwa sababu alikuwa mkarimu na mwenye bidii, na zaidi ya yote, alikuwa mwanamke wa kiroho. Aliamini kabisa mafundisho ya Yesu, na hakuwa na shaka hata kidogo kwamba Yesu alikuwa Masihi aliyeahidiwa. (Yoh. 11:21-27) Hata hivyo, Martha hakuwa mkamilifu kama tu wanadamu wengine. Wakati fulani, Yesu alipowatembelea nyumbani, Martha alimkasirikia dada yake kwa sababu ya jambo ambalo alifikiri si sawa na akamwambia Yesu amrekebishe. Martha alisema hivi: “Bwana, hujali kwamba dada yangu ameniacha peke yangu kushughulikia mambo? Kwa hiyo, mwambie aje anisaidie.” (Soma Luka 10:38-42.) Simulizi hilo linatufundisha nini?
-
-
Mtumikie Yehova Bila KukengeukaMnara wa Mlinzi—2015 | Oktoba 15
-
-
4 Hata hivyo, Martha alikuwa na shughuli nyingi akitayarisha mlo na kufanya kazi nyingine ili tukio hilo liwe la pekee. Lakini mambo hayo yalimsababishia mahangaiko yasiyo ya lazima, na kufanya amkasirikie Maria. Yesu alitambua kwamba Martha anahangaikia mambo mengi, hivyo akamwambia hivi kwa upole: “Martha, Martha, wewe unahangaika na kusumbuka juu ya mambo mengi.” Kisha akasema kwamba hata mlo mmoja tu ungetosha. Halafu Yesu akamgeukia Maria na kumwondolea wasiwasi kwa kusema hivi: “Maria alichagua fungu jema, nalo halitaondolewa kwake.” Baada ya muda mfupi, Maria angesahau chakula walichokula wakati huo, lakini hangesahau kamwe pongezi na mambo aliyofundishwa na Yesu. Zaidi ya miaka 60 baadaye, mtume Yohana aliandika hivi: “Yesu alimpenda Martha na dada yake.” (Yoh. 11:5) Maneno hayo yanaonyesha kwamba Martha alikubali kurekebishwa na Yesu na akajitahidi kumtumikia Yehova kwa uaminifu maishani mwake.
-