-
Yehova Anawapa “Roho Takatifu Wale Wanaomwomba”Mnara wa Mlinzi—2006 | Desemba 15
-
-
4 Yesu alisema: “Ni nani kati yenu aliye na rafiki naye amwendee katikati ya usiku na kumwambia, ‘Rafiki, nikopeshe mikate mitatu, kwa sababu rafiki yangu amenijia sasa hivi kutoka safarini nami sina kitu cha kuweka mbele yake’? Na huyo aliye ndani ajibu na kusema, ‘Acha kunisumbua. Tayari mlango umefungwa, na watoto wangu wachanga wako pamoja nami kitandani; siwezi kuamka nikupe chochote.’ Ninawaambia ninyi, Ijapokuwa hataamka ampe chochote kwa sababu ya kuwa rafiki yake, hakika kwa sababu ya kudumu kwake kwa ujasiri, ataamka na kumpa vitu anavyohitaji.” Kisha, Yesu alieleza jinsi mfano huo unavyohusiana na sala. Alisema hivi: “Basi ninawaambia ninyi, Endeleeni kuomba, nanyi mtapewa; endeleeni kutafuta, nanyi mtapata; endeleeni kupiga hodi, nanyi mtafunguliwa. Kwa maana kila mtu anayeomba hupokea, na kila mtu anayetafuta hupata, na kila mtu anayepiga hodi hufunguliwa.”—Luka 11:5-10.
-
-
Yehova Anawapa “Roho Takatifu Wale Wanaomwomba”Mnara wa Mlinzi—2006 | Desemba 15
-
-
6. Katika siku za Yesu, watu walikuwa na maoni gani kuhusu desturi ya kuwakaribisha wageni?
6 Yesu hatuonyeshi tu jinsi tunavyopaswa kusali, yaani, kwa ujasiri na bila kuacha, lakini anatuonyesha pia kwa nini tunapaswa kufanya hivyo. Ili kuelewa vizuri somo hilo, tunapaswa kuchunguza jinsi wale waliosikiliza mfano wa Yesu kuhusu yule mtu aliyeomba bila kuacha walivyoona desturi ya kuwakaribisha wageni. Masimulizi mengi katika Maandiko yanaonyesha kwamba katika nyakati za Biblia, desturi ya kuwatunza wageni ilichukuliwa kwa uzito, hasa na watumishi wa Mungu. (Mwanzo 18:2-5; Waebrania 13:2) Kukosa kuwakaribisha wageni lilikuwa jambo la aibu. (Luka 7:36-38, 44-46) Tukiwa na hilo akilini, acheni tuchunguze tena mfano wa Yesu.
7. Kwa nini yule mtu katika mfano wa Yesu haoni haya kumwamsha rafiki yake?
7 Yule mtu anayetajwa katika mfano anapokea mgeni katikati ya usiku. Mtu huyo anahisi kwamba ni lazima ampe mgeni wake chakula, lakini ‘hana kitu cha kuweka mbele yake.’ Kwa maoni yake, hilo ni jambo linalohitaji kufanywa haraka! Kwa vyovyote vile, lazima apate mkate. Kwa hiyo, anaenda kwa rafiki yake, na bila kuona haya anamwamsha. Naye anampaazia sauti hivi, “Rafiki, nikopeshe mikate mitatu.” Anamwomba bila kuacha mpaka anapopata kile anachohitaji. Hivyo basi, yeye ni mkaribishaji mzuri kwa kuwa sasa ana mikate mkononi mwake.
Kuomba Kadiri ya Uhitaji Wetu
8. Ni nini ambacho kitatuchochea tuendelee kusali ili tupewe roho takatifu?
8 Mfano huo unatupa sababu gani ya kusali bila kuacha? Mtu huyo aliendelea kuomba apewe mikate kwa sababu alihisi kwamba ilikuwa lazima apate mikate hiyo ili atimize wajibu wake akiwa mkaribishaji. (Isaya 58:5-7) Kama hangekuwa na mikate hiyo, hangetimiza wajibu huo vizuri. Vivyo hivyo, tunaendelea kusali kwa Mungu, tukimwomba roho yake kwa kuwa tunatambua kwamba ni lazima tuwe na roho ya Mungu ili tutimize huduma yetu tukiwa Wakristo wa kweli. (Zekaria 4:6) Bila roho hiyo, hatutafanikiwa. (Mathayo 26:41) Je, unaona jambo la maana tunalojifunza kutokana na mfano huo? Tukitambua kwamba tunahitaji sana roho ya Mungu, inaelekea kuwa tutaendelea kuomba ili tupewe roho hiyo.
9, 10. (a) Toa mfano ambao unaonyesha kwa nini tunahitaji kuendelea kumwomba Mungu roho yake. (b) Tunapaswa kujiuliza swali gani, na kwa nini?
9 Ili kuona jinsi mfano huo unavyotuhusu leo, wazia kwamba mtu fulani katika familia yenu anakuwa mgonjwa katikati ya usiku. Je, ungemwamsha daktari na kumwomba akusaidie? Hungefanya hivyo ikiwa mtu huyo si mgonjwa sana. Hata hivyo, ikiwa angekuwa na mshtuko wa moyo, hungeona haya kumwamsha daktari. Kwa nini? Kwa sababu unakabili hali ya hatari. Unatambua kwamba ni lazima upate msaada wa daktari. Mtu huyo anaweza kufa usipoomba msaada. Vivyo hivyo, Wakristo wa kweli wanaendelea kukabili hali ya hatari. Kwa kweli, Shetani anazunguka-zunguka kama “simba anayenguruma,” akijaribu kutumeza. (1 Petro 5:8) Ili tuendelee kuwa hai kiroho, ni lazima kabisa tupate msaada wa roho ya Mungu. Tusipomwomba Mungu msaada, tunaweza kupata msiba. Hivyo, kwa ujasiri tunaendelea bila kuacha kumwomba Mungu atupe roho yake takatifu. (Waefeso 3:14-16) Ni kwa kufanya hivyo tu ndipo tutaendelea kuwa na nguvu zinazohitajiwa ili ‘kuvumilia mpaka mwisho.’—Mathayo 10:22; 24:13.
-