-
Alikata “Kauli Moyoni Mwake”Igeni Imani Yao
-
-
10 Maria na Yosefu walipata kijiji hicho kikiwa kimejaa watu. Wengi walikuwa wamefika kabla yao ili kuandikishwa, hivyo, hawakupata nafasi katika chumba cha wageni.b Walilazimika kulala zizini. Tunaweza kuwazia jinsi Yosefu alivyohangaika alipomwona mkewe akiwa na maumivu makali yaliyozidi kuongezeka. Hapo ndipo uchungu wake wa kuzaa ulianzia.
11. (a) Kwa nini wanawake wanaelewa vizuri hali iliyomkabili Maria? (b) Yesu alikuwa “mzaliwa wa kwanza” katika njia gani?
11 Wanawake wanaelewa vizuri jinsi Maria alivyohisi. Miaka 4,000 hivi mapema, Yehova alikuwa ametabiri kwamba wanawake wangezaa kwa uchungu kwa sababu walirithi dhambi. (Mwa. 3:16) Inaelekea Maria pia alizaa kwa uchungu. Simulizi la Luka halitaji uchungu ambao Maria alipata, linasema tu: “Akamzaa mwana wake, mzaliwa wa kwanza.” (Luka 2:7) Ndiyo, alikuwa “mzaliwa wa kwanza” wa watoto saba hivi wa Maria. (Marko 6:3) Hata hivyo, mwana huyo angekuwa wa pekee. Mbali na kuwa mwana wake mzaliwa wa kwanza, pia alikuwa “mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote” vya Yehova, Mwana mzaliwa-pekee wa Mungu!—Kol. 1:15.
12. Maria alimlaza mtoto wapi, na kwa nini hali ilikuwa tofauti na jinsi inavyoonyeshwa kwenye michoro na michezo ya kuigiza?
12 Sasa simulizi hilo linataja jambo linalojulikana sana: “Akamfunga vitambaa na kumlaza katika hori.” (Luka 2:7) Ulimwenguni pote michoro, na michezo ya kuigiza kuhusu kuzaliwa kwa Yesu inarembesha sana tukio hilo. Hata hivyo, fikiria mambo haya hakika. Hori ni chombo cha kulishia wanyama wa kufugwa. Kumbuka, familia hiyo ilikuwa katika zizi ambalo kwa kawaida halikuwa na hewa wala mazingira safi. Ni wazazi gani ambao wangechagua mtoto wao azaliwe mahali kama hapo ikiwa wangepata mahali bora? Wazazi wengi hutaka kuwapa watoto wao vitu bora. Basi lazima Maria na Yosefu walitaka kumpa Mwana wa Mungu kilicho bora zaidi!
13. (a) Maria na Yosefu walifanyaje yote waliyoweza kulingana na hali yao? (b) Leo, wazazi wenye hekima wanawezaje kutanguliza mambo ya kiroho kama Yosefu na Maria?
13 Hata hivyo, hawakuruhusu hali yao iwakatishe tamaa; walijitahidi wawezavyo. Kwa mfano, ona kwamba Maria alimtunza mtoto huyo kwa kumfunga kwa vitambaa, kisha akamlaza kwa uangalifu ndani ya hori ili alale, na kuhakikisha kwamba alikuwa salama. Hata katika hali hiyo ngumu, Maria alijitahidi kumwandalia mtoto wake kilicho bora. Pia, yeye na Yosefu walijua kwamba jambo muhimu zaidi ambalo wangemfanyia mtoto huyo ni kumtunza kiroho. (Soma Kumbukumbu la Torati 6:6-8.) Leo, wazazi wenye hekima wanatanguliza mambo ya kiroho wanapowalea watoto wao katika ulimwengu huu uliopotoka.
-
-
Alikata “Kauli Moyoni Mwake”Igeni Imani Yao
-
-
b Ilikuwa kawaida kwa miji kuwa na chumba cha kulala kwa ajili ya wasafiri.
-