-
Je, Wewe Ni “Tajiri Kwa Mungu”?Mnara wa Mlinzi—2007 | Agosti 1
-
-
7. Mtu anayetajwa katika mfano wa Yesu alitatua tatizo lake jinsi gani?
7 Tukichunguza tena mfano wa Yesu, yule mtu tajiri alifanya nini wakati shamba lake lilipozaa vizuri hivi kwamba hakuwa na mahali pa kuweka mavuno yake? Aliamua kubomoa maghala ambayo alikuwa nayo na kujenga makubwa zaidi ili aweke akiba nafaka yake yote ya ziada na vitu vyema. Inaonekana alitosheka na mpango huo na kujihisi akiwa salama hivi kwamba akawaza: “Nami nitaiambia nafsi yangu: ‘Nafsi yangu, una vitu vyema vingi vilivyokusanywa kwa miaka mingi; starehe, ule, unywe, na kujifurahisha.’”—Luka 12:19.
Kwa Nini ‘Hakuwa na Akili’?
8. Mtu anayetajwa katika mfano wa Yesu alipuuza jambo gani la maana?
8 Hata hivyo, kama Yesu alivyoonyesha, mipango ya mtu huyo tajiri ilimfanya ahisi usalama usio wa kweli. Ingawa huenda mipango hiyo ilionekana kuwa mizuri, mtu huyo alipuuza jambo fulani la maana, yaani, mapenzi ya Mungu. Mtu huyo alikuwa akijifikiria mwenyewe tu, jinsi ambavyo angestarehe na kula, kunywa, na kujifurahisha. Alifikiri kwamba kwa sababu alikuwa na ‘vitu vingi vyema’ angeishi pia “miaka mingi.” Lakini inasikitisha kwamba mambo hayakuwa hivyo. Kama tu Yesu alivyosema mapema, “hata wakati mtu ana vitu vingi uzima wake hautokani na vitu alivyo navyo.” (Luka 12:15) Usiku huohuo, jitihada zote za mtu huyo zilifikia mwisho ghafula, kwa sababu Mungu alimwambia hivi: “Wewe usiye na akili, usiku huu wanadai nafsi yako kutoka kwako. Basi, vitu ulivyoviweka akiba vitakuwa vya nani?”—Luka 12:20.
-
-
Je, Wewe Ni “Tajiri Kwa Mungu”?Mnara wa Mlinzi—2007 | Agosti 1
-
-
10. Kwa nini kuwa na “vitu vyema vingi” si uhakikisho wa kuishi “miaka mingi”?
10 Tunapaswa kufikiria kwa uzito somo la mfano huo. Je, tunaweza kuwa kama mtu aliye katika mfano huo na kufanya kazi kwa bidii sana ili kuhakikisha kwamba tuna “vitu vyema vingi” lakini tukose kufanya yale tunayohitaji kufanya ili kuwa na tumaini la kuishi “miaka mingi”? (Yohana 3:16; 17:3) Biblia inasema hivi: “Vitu vyenye thamani havitakuwa na faida yoyote siku ya ghadhabu,” na “anayetegemea utajiri wake—yeye mwenyewe ataanguka.” (Methali 11:4, 28) Kwa hiyo, Yesu alimalizia mfano wake kwa himizo hili: “Hivyo ndivyo huwa kwa mtu anayejikusanyia mwenyewe hazina lakini si tajiri kwa Mungu.”—Luka 12:21.
-