-
Jifunze Kutoka kwa NikodemoMnara wa Mlinzi—2002 | Februari 1
-
-
Miezi sita tu baada ya Yesu kuanza huduma yake duniani, Nikodemo anamtambua ‘kuwa mwalimu kutoka kwa Mungu.’ Kwa kuvutiwa na miujiza ambayo Yesu alikuwa amefanya karibuni huko Yerusalemu kwenye Sikukuu ya Kupitwa ya mwaka wa 30 W.K., Nikodemo anakuja usiku kukiri kwamba anamwamini Yesu na pia kujifunza mengi zaidi kuhusu mwalimu huyo. Hivyo, Yesu anamfunza Nikodemo ukweli muhimu kuhusu uhitaji wa ‘kuzaliwa tena’ ili kuingia katika Ufalme wa Mungu. Katika pindi hiyo pia Yesu anasema maneno haya: “Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akatoa Mwana mzaliwa-pekee wake, ili kila mtu anayedhihirisha imani katika yeye asipate kuangamizwa bali awe na uhai udumuo milele.”—Yohana 3:1-16.
Nikodemo ana taraja zuri kama nini! Anaweza kuwa mshiriki wa karibu wa Yesu na kujionea moja kwa moja mambo mbalimbali yanayotukia katika maisha ya Yesu duniani. Akiwa mtawala wa Wayahudi na mwalimu wa Israeli, Nikodemo analijua vizuri Neno la Mungu. Pia ana ufahamu mwingi kwa kuwa anaweza kutambua kwamba Yesu ni mwalimu aliyetumwa na Mungu. Nikodemo anapendezwa na mambo ya kiroho, na ni mnyenyekevu isivyo kawaida. Ni jambo gumu kama nini kwa mshiriki wa mahakama kuu zaidi ya Wayahudi kukiri kwamba mwana wa seremala tu ni mtu aliyetumwa na Mungu! Sifa hizo zote ni muhimu sana ili mtu awe mwanafunzi wa Yesu.
-
-
Jifunze Kutoka kwa NikodemoMnara wa Mlinzi—2002 | Februari 1
-
-
Kwanza kabisa, Yohana anasema kwamba mtawala huyo wa Wayahudi “alimjia [Yesu] wakati wa usiku.” (Yohana 3:2) Msomi mmoja wa Biblia anadokeza: “Nikodemo alikuja usiku si kwa sababu aliogopa, bali kwa sababu alitaka kuepuka umati ambao ungekatiza mazungumzo yake pamoja na Yesu.” Hata hivyo, Yohana anamtaja Nikodemo kuwa “yule mtu aliyemjia [Yesu] usiku mara ya kwanza” na katika muktadha huohuo anamtaja Yosefu wa Arimathea kuwa “mwanafunzi wa Yesu lakini wa siri kutokana na kuhofu kwake Wayahudi.” (Yohana 19:38, 39) Kwa hiyo, inaelekea kwamba Nikodemo alimjia Yesu usiku kwa ‘kuhofu Wayahudi,’ kama vile wengine walioishi wakati huo walivyohofu kuhusianishwa na Yesu.—Yohana 7:13.
-