-
Kuzaliwa Upya—Je, Ni Muhimu?Mnara wa Mlinzi—2009 | Aprili 1
-
-
Ona jinsi Yesu alivyokazia umuhimu wa kuzaliwa upya alipozungumza na Nikodemo. Alisema: “Mtu asipozaliwa tena, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.” (Yohana 3:3) Maneno “asipozaliwa tena” na “hawezi” yanaonyesha kwamba ni lazima mtu azaliwe upya. Kwa mfano: Mtu akisema, “Jua lisipowaka, hakuwezi kuwa na mwangaza wa mchana,” anamaanisha kwamba ni lazima jua liwake ili kuwe na mwangaza wa mchana. Vivyo hivyo, Yesu alisema kwamba kuzaliwa tena ni jambo la lazima kabisa ili kuuona Ufalme wa Mungu.
-
-
Kuzaliwa Upya—Je, Ni Uamuzi wa Mtu Binafsi?Mnara wa Mlinzi—2009 | Aprili 1
-
-
Unaposoma kwa makini maneno ya Yesu, utaona kuwa yeye hakufundisha kwamba mtu binafsi ndiye anayechagua kuzaliwa upya. Kwa nini tunasema hivyo? Neno la Kigiriki linalotafsiriwa ‘kuzaliwa tena’ linaweza pia kutafsiriwa “kuzaliwa kutoka juu.”a Hivyo, mtu anazaliwa upya “kutoka juu,” yaani, “kutoka mbinguni,” au “kutoka kwa Baba.” (Yohana 19:11; Yakobo 1:17) Ndiyo, Mungu ndiye anayefanya mtu azaliwe upya.—1 Yohana 3:9.
-
-
Kuzaliwa Upya—Je, Ni Uamuzi wa Mtu Binafsi?Mnara wa Mlinzi—2009 | Aprili 1
-
-
a Katika Biblia kadhaa, Yohana 3:3 limetafsiriwa kwa njia hiyo. Kwa mfano, A Literal Translation of the Bible inasema: “Mtu asipozaliwa kutoka juu, hawezi kuuona Ufalme wa Mungu.”
-